Monday, June 13, 2016

Soka

kTETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU 13.06.2016 Manchester United wapo tayari kutoa pauni milioni 79 kumsajili kiungo wa Paris St-Germain, Marco Verratti (Corriere dello Sport, via Daily Star), Zlatan Ibrahimovic ameahidi kutaja klabu anayokwenda "hivi karibuni" huku tetesi zikiendelea kuashiria kuwa ni Old Trafford (Daily Express), Pep Guardiola anataka kuwasajili John Stones, 22, wa Everton na Aymeric Laporte, 22, katika uhamisho utakaogharimu takriban pauni milioni 85 (Manchester Evening News), Liverpool wametoa pauni milioni 9.5 kumtaka kiungo wa Udinese Piotr Zielinski, 22 (Guardian), Liverpool wanapanga kumfuatilia beki wa River Plate Gabriel Mercado, baada ya meneja Jurgen Klopp kumtazama mchezaji huyo akiichezea Argentina kwenye michuano ya Copa America (Sunday People), Tottenham wanakaribia kukamilisha uhamisho wa kungo wa Southampton, Victor Wanyama kwa pauni milioni 12 (Daily Star), Ronald Koeman anataka kumsajili kipa wa Southampton Fraser Foster mara atakapothibitishwa kuwa meneja mpya wa Everton, Sunday Express). Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.

Sunday, June 12, 2016

Siku ya watu wenye ualbino

Leo ni siku ya Watu Wenye Ualbino "Hii siku ilianza kuanzimishwa miaka mingi iliyopita lakini Umoja Wa Mataifa mwaka juzi ( 2014) uliamua tarehe 13 Juni kila mwaka iwe ni Siku ya kuadhimisha Watu Wenye Ualbino Duniani mara nyingi Umoja wa Mataifa huwa na utaratibu wa kuweka siku maalum kwa makundi fulani ya watu wenye historia kama siku ya Watoto, Mwanamke n.k na sasa suala la watu wenye Ualbino limekuwa ni suala la Haki Za Binadamu, basi Umoja Wa Mataifa wakaamua siku hii iwe maalum kwa ajili ya Watu Wenye Ualbino Duniani kikubwa zaidi ni kwa ajili ya kutoa uelewa kuhakikisha kwamba watu we ye Ualbino wanapata nafasi yao wanayoistahili katika maisha ya kawaida ya mwanadamu, maadhimisho haya yanafanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja" Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Dkt. Abdallah Possi #PowerBreakFast