Sunday, June 12, 2016

Siku ya watu wenye ualbino

Leo ni siku ya Watu Wenye Ualbino "Hii siku ilianza kuanzimishwa miaka mingi iliyopita lakini Umoja Wa Mataifa mwaka juzi ( 2014) uliamua tarehe 13 Juni kila mwaka iwe ni Siku ya kuadhimisha Watu Wenye Ualbino Duniani mara nyingi Umoja wa Mataifa huwa na utaratibu wa kuweka siku maalum kwa makundi fulani ya watu wenye historia kama siku ya Watoto, Mwanamke n.k na sasa suala la watu wenye Ualbino limekuwa ni suala la Haki Za Binadamu, basi Umoja Wa Mataifa wakaamua siku hii iwe maalum kwa ajili ya Watu Wenye Ualbino Duniani kikubwa zaidi ni kwa ajili ya kutoa uelewa kuhakikisha kwamba watu we ye Ualbino wanapata nafasi yao wanayoistahili katika maisha ya kawaida ya mwanadamu, maadhimisho haya yanafanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja" Naibu Waziri ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Ajira, Vijana na Walemavu, Mhe. Dkt. Abdallah Possi #PowerBreakFast

No comments:

Post a Comment