Thursday, August 17, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 18.08.2017
Manchester United wanataka kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar. (Daily Record)

Manchester United bado wana matumaini ya kukamilisha usajili wa Ivan Perisic. (Mirror)

Tottenham wamefikia makubaliano ya kimsingi ya kumsajili Davinson Sanchez, 21, kutoka Ajax kwa pauni milioni 28 na milioni 14 zaidi kama marupurupu. (Independent)

Manchester City wapo tayari kuwapa West Brom pauni milioni 22 ili kumsajili nahodha wao Jonny Evans, 29, baada ya dau la pauni milioni 18 kukataliwa, na watampa mara mbili ya mshahara wa pauni 75,000 kwa wiki anaolipwa sasa. (Mirror)

Dau la Chelsea la pauni milioni 62 kumtaka beki wa Juventus Alex Sandro, limekataliwa. (Mirror)

Chelsea wanajiandaa kumuuza Diego Costa kwa hasara. (Sun)

Mkurugenzi wa michezo wa Barcelona Robert Fernandez amesema itakuwa “vigumu” kumsajili kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, kwa sababu hana kipengele cha uhamisho kwenye mkataba wake. (Liverpool Echo)

Barcelona “watapigana” mpaka siku ya mwisho ya usajili ili kumsajili Philippe Coutinho kutoka Liverpool. (Telegraph)
Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa, 28, amesema hatorudi Stamford Bridge na anataka kujiunga na Atletico Madrid. (Telegraph)

Everton huenda wakamtaka Diego Costa kwa mkopo. (Sun)

Beki wa Tottenham Kevin Wimmer, 24, anazungumza na Stoke City kuhusu uhamisho wake wa pauni milioni 15. (Telegraph)

Stoke City pia wanataka kumsajili Kevin Wimmer kutoka Spurs. (Stoke Sentinel)

Beki wa Arsenal Gabriel, 26, anakaribia kujiunga na Valencia kwa pauni milioni 10. (Evening Standard)

Paris Saint-Germain bado wanataka kumsajili kiungo mkabaji wa Monaco, Fabinho, 23. (L’Equipe)

Kiungo wa PSG Blaise Matuidi, 30, amekamilisha vipimo vya afya Juventus, lakini timu hizo mbili bado hazijakubaliana jinsi ada ya uhamisho itakavyolipwa, huku meneja wa PSG Unai Emery akisema hakutaka kumuuza mchezaji huyo. (Le Parisien)

Wakurugenzi wa Borussia Dortmund wamesema Barcelona “hata hawapo karibu” katika kufikia dau la mshambuliaji wake Ousmane Dembele, 20. (Kicker)

Fiorentina wamemwambia mshambuliaji wake Nikola Kalinic, 29, anayenyatiwa na AC Milan kuwa atapigwa faini kwa kutotokea mazoezini siku ya Alhamisi. (Sun)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumaa Kareem.

Monday, August 14, 2017

Tetesi za soka ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU 14.08.2017
Chelsea wanafikiria kutaka kumsajili mchezaji anayenyatiwa na Manchester United Ivan Perisic , 28, kutoka Inter Milan. (Mirror)

Barcelona wanataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, 26. (Diario Gol)

Cezar Azpilicueta, 27, anadhani Chelsea wanahitaji kusajili wachezaji kadhaa zaidi kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Evening Standard)

Chelsea wapo tayari kupanda dau la pauni milioni 50 wiki hii kumtaka beki wa kati wa Southampton Virgil van Dijk na kuwapiku Liverpool. (Daily Star)

Manchester United watakuwa tayari kulipa pauni milioni 36.5 kumsajili kiungo wa Barcelona Sergi Roberto, 25, ikiwa mchezaji huyo atataka kuondoka Uhispania. (Don Balon)

Manchester United wanakaribia kufikia makubaliano na Oliveirense ya Ureno kumsajili mshambuliaji Bruno Amorim, 19. (Daily Mail)

Antoinne Griezmann, 26, atachukizwa na hatua ya Atletico Madrid kumuuza kipa wake Jan Oblak na huenda akafikiria kuhamia Manchester United. (Don Ballon)

Leicester City watakataa dau la Roma la pauni milioni 31 la kumtaka Rirad Mahrez. Leicester wanataka pauni milioni 50. (Mirror)

Mkurugenzi mkuu wa Juventus Beppe Marotta amesema wanamtaka kiungo anayesakwa na Liverpool Naby Keita, 22, anayechezea RB Leipzig. (La Gazzetta dello Sport)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema anahitaji kuimarisha kikosi chake kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Liverpool Echo)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anafikiria kumsajili mshambuliaji wa Napoli Lorenzo Insigne, kuchukua nafasi ya Philippe Coutinho anayenyatiwa na Barcelona. (Express)

Barcelona hawatokata tamaa ya kumsajili Philippe Coutinho, 25, kutoka Liverpool, na wapo tayari kutoa pauni milioni 137 kumshawishi mchezaji huyo. (The Sun)

Mshambuliaji wa Real Madrid Marco Asensio atakuwa na mazungumzo ya dharura na klabu yake kuhusiana na kutaka kuhamia Arsenal. (The Mirror)

Tottenham wataongeza bidii ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Lazio Keita Balde, 22, ambaye hakupangwa katika kikosi cha kwanza kwenye mechi iliyopita. (Mirror)

Winga wa PSG Jese Rodriguez, 24, amekataa kwenda Fiorentina kwa mkopo na anajiandaa kwenda Stoke kwa mkopo. (Sun)

Schalke wanazungumza na Chelsea kuhusu kumchukua tena kwa mkopo beki Baba Rahman, 23. (Sky Sports)

Newcastle wameongeza bidii ya kujaribu kumsajili kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25, baada ya mchezaji huyo kuachwa katika kikosi kilichocheza dhidi ya Leicester. (Sun)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.

Sunday, August 13, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 13.08.2017
Paris Saint-Germain wamekamilisha usajili wa Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco kwa pauni milioni 173. (The Times)

Real Madrid watawapiku Barcelona katika kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20. (RAC-1)

Manchester United wametupilia mbali dau la Tottenham la kumtaka Anthony Martial, 21. (RMC Sport)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atataka kumsajili mshambuliaji wa Napoli Lorenzo Insigne, 26, iwapo Philippe Coutinho, 25, atalazimisha kuondoka na kwenda Barcelona. (Sunday People)

Barcelona watarejea Liverpool na dau la pauni milioni 100 kumtaka Philippe Coutinho. (Sunday Express)

Chelsea wiki hii watapanda dau la pili la takriban pauni milioni 25 kumtaka kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater, 27, baada ya pauni milioni 15 za awali kukataliwa. (Sunday Telegraph)

Real Madrid wamekiri kukata tamaa ya kutaka kumsajili kipa wa Manchester United David De Gea msimu huu. (Sunday Express)

Barcelona wamemsajili kiungo wa zamani wa Tottenham, Paulinho, 29, kwa pauni milioni 36.6 kutoka Guangzhou Evergrande ya China. (Mail on Sunday)

Paris Saint-Germain huenda wakatumia zaidi ya pauni milioni 54.9 kumsajili beki wa Monaco Fabinho, 23. (ESPN)

Kiungo Mjerumani Mesut Ozil, 28, hataki kubakia Arsenal na anataka kulazimisha uhamisho wa kwenda Barcelona. (Don Balon)

Tottenham watamwaga fedha kabla ya dirisha la usajili kufungwa, wakianza na kupanda dau la kumtaka kiungo wa Everton Ross Barkley, 23. (Sunday Telegraph)

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anahoji kwanini wanamfuatilia Ross Barkley, yeye anawataka zaidi kiungo wa Celta Vigo Pape Cheikh Diop, 20, na beki wa Ajax Davinson Sanchez, 21. (Sun on Sunday)

Ajax wamekataa dau la pauni milioni 36.6 kutoka Tottenham la kumtaka Davinson Sanchez, na amepewa mkataba mpya ili kumshawishi asalie Ajax. (De Telegraaf)

Chelsea watakuwa tayari kumuuza Eden Hazard, 26, iwapo Barcelona watakuwa tayari kutoa pauni milioni 110. (Diario Gol)

Manchester United wameanza tena mazungumzo na Inter Milan ya kutaka kumsajili winga Ivan Perisic, 28, na wanakaribia kutoa kitita cha pauni milioni 48 wanachotaka Inter. (Sunday Mirror)

Chelsea wana wasiwasi kuwa mshambuliaji wake Diego Costa, 28, amenenepa sana baada ya kwenda likizo ya mapumziko Brazil na huenda ikawa vigumu kumuuza. (Sunday Times)

Diego Costa huenda akapigwa faini na Chelsea kwa kushindwa kurejea mazoezini wiki mbili zilizopita. (Daily Star)

Liverpool wamemuambia Emre Can, 23, kuwa haendi popote licha ya Juventus kujipanga kutoa pauni milioni 23 kumtaka kiungo huyo Mjerumani ambaye amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake. (Sunday Mirror)

Kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, hatimaye atakamilisha uhamisho wake kwenda Everton wiki hii, na hivyo kufanya Swansea kumfuatilia kiungo wa West Brom Nacer Chadli, 28, na huenda kusababisha Tottenham kumsajili Ross Barkley, 23, kutoka Everton. (Sunday People)

Meneja wa Everton Ronald Koeman, baada ya kumsajili Gylfi Sigurdsson atataka kumsajili mshambuliaji wa Fiorentina Nikola Kalinic, 29. (Sunday Express)

Mshambuliaji wa kimataifa wa Croatia na Fiorentina Nikola Kalinic, 29, anataka kwenda AC Milan. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Antoinne Griezmann, 26, huenda akaondoka Atletico Madrid, iwapo kipa Jan Oblak, 24, atauzwa kwenda PSG. (Don Balon)

Kiungo mshambuliaji wa Real Madrid Marco Asensio, 21, anataka kutumia nafasi ya Arsenal kumnyatia ili apate mkataba mpya Real. (Diario Balon)

Arsenal wamekata tamaa ya kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar, 21, na sasa meneja Arsene Wenger anatazama zaidi kupunguza wachezaji asiowahitaji ili kupunguza gharama za mishahara. (Mail on Sunday)

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez anataka kumsajili kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25. (Sun on Sunday)

Tukutane baadaye katika BBC Ulimwengu wa Soka ambapo tutakutangazia mechi ya Manchester United v West Ham United.

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumapili njema.

Friday, August 11, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 11.08.2017
Arsenal wamempa Alexis Sanchez mkataba mpya na mshahara wa pauni 300,000 kwa wiki na kumfanya mchezaji anayelipwa zaidi katika EPL. (Daily Mail)

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekiri kuwa “hana uhakika sana” kama ataweza kumshawishi Alexis Sanchez kukubali kusaini mkataba mpya. (SFR)

Juventus wanajiandaa kutoa pauni milioni 23 kujaribu kuishawishi Liverpool kumuuza Emre Can. (Gazzetta dello Sport)

Juventus nao wameingia katika mbio za kutaka kumsajili Sergi Roberto kutoka Barcelona, ambaye pia Manchester United na Chelsea zinamtaka. (Sport.es)

West Ham wamepanda dau la pauni milioni 27.1 kumtaka kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 25. (Daily Telegraph)

Barcelona hawatakuwa na uwezo wa kumnunua Philippe Coutinho kutoka Liverpool iwapo watafanikiwa kumsajili Ousmane Dembele, 20, kutoka Borussia Dortmund, kwa mujibu wa mwandishi wa ha1ba12ri za michezo Graham Hunter. (BBC Radio 5 Live)

Barcelona wapo tayari kuwapa Liverpool Ivan Rakitic kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Philippe Coutinho. (Don Balon)

Barcelona wanamtaka kiungo mchezeshaji wa Real Madrid Marco Asensio na wapo tayari kutoa pauni milioni 72. (Diario Gol)

Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Lexy anakabiliwa na sekeseke la wachezaji kudai kuongezewa mishahara baada ya beki Danny Rose kushutumu sera za klabu hiyo. (Daily Mirror)

Danny Rose alipokelewa kwa shangwe na wachezaji wenzake baada ya kuweka wazi mtazamo wa Tottenham, huku wachezaji wengine wakitishia na wao kuweka mambo hadharani. (Daily Mirror)

Wachezaji nyota wa Tottenham wanataka kuondoka kwa sababu ya sera ya malipo ya klabu hiyo. (Daily Mail)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anatafuta beki wa kushoto na Danny Rose wa Tottenham ni mmoja wa wachezaji anaowafuatilia. (Daily Record)

Meneja wa Everton Ronald Koeman ameiambia Tottenham kuwa hawataweza kumsajili kiungo Ross Barkley kwa bei rahisi. (Daily Star)

Arsenal wanaamini kuwa wamefanikiwa katika mazungumzo ya kumshawishi Mesut Ozil kubakia Emirates baada ya kumpa mkataba wa mshahara wa pauni 225,000 kwa wiki, na mchezaji huyo ameonesha dalili za kukubali. (Sun)
PSG wapo tayari kuwapa Atletico Madrid Javier Pastore katika mkataba wa kumsajili kipa Jan Oblak, 24. (AS)

Real Madrid wamekuwa na mazungumzo ya siri na Juventus kuhusiana na mshambuliaji Paulo Dybala, 23, ambaye pia anasakwa na Barcelona. (Don Balon)

Juventus wanamtaka Kevin Strootman kabla ya dirisha la usajili kufungwa, huku Roma wakisema bei yake ni euro milioni 45. (Tuttosport)

Arsene Wenger amesema meneja wa Chelsea Antonio Conte awarejeshe wachezaji wanaocheza nje kwa mkopo kama ana wasiwasi na idogo wa kikosi chake. (Times)

Msimu wa EPL unaanza rasmi leo. Arsenal wanacheza na Leicester City saa nne kasorobo usiku huu kwenye uwanja wa Emirates. Matokeo ya mchezo huo utayapata hapa hapa.

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumaa Kareem.

Thursday, August 10, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 10.08.2017
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anataka kusajili angalau mchezaji mmoja zaidi kabla ya dirisha la usajili kufungwa, huku beki wa kushoto Danny Rose, 27, na winga wa Inter Milan Ivan Perisic wakiendelea kunyatiwa na United. (Manchester Evening News)

Jose Mourinho ameitaka Manchester United kupanda dau la pauni milioni 100 kumtaka Gareth Bale wa Real Madrid. (The Sun)

Danny Rose amesema hana mpango wa kuondoka Tottenham, lakini anaamini anastahili kulipwa zaidi kuliko anavyolipwa sasa. (Sun)

Danny Rose ameitaka Tottenham kusajili wachezaji wenye majina makubwa. (Sun)

Tottenham wapo tayari kutoa pauni milioni 55 kumtaka beki wa Ajax Davinson Sanchez. (The Sun)

Paris Saint-Germain wanakaribia kumsajili mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, kwa pauni milioni 163, na tayari wamekamilisha mkataba na Fabinho, 23, pia wa Monaco. (Daily Record)

Iwapo Kylian Mbappe ataondoka, Monaco wataamua kumfuatilia mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia, Carlos Bacca anayeichezea AC Milan. (Caracol Radio)

Chelsea wamepanda dau la pauni milioni 35 kumtaka kiungo mshambuliaji wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Daily Star)

Chelsea wanazidi kuonekana kuwa na nafasi zaidi ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Everton Ross Barlkey, ambaye pia ananyatiwa na Tottenham. (Daily Telegraph)

Arsenal wana wasiwasi kuwa mshambuliaji wake Alexis Sanchez, 28, huenda akataka kulazimisha uhamisho wake kuondoka Emirates. (Daily Mirror)

Barcelona watarejea tena Liverpool na dau la nne la kumtaka kiungo mshambuliaji kutoka Brazil Philippe Coutinho, 25. (Daily Mail)

Barcelona na Atletico Madrid wanapambana katika kutaka kumsajili Lautaro Martinez anayechezea Racing Club ya Argentina. (El Grafico)

Barcelona wameambiwa walipe pauni milioni 135 kama wanataka kumsajili Ousmane Dembele, 20, wa Borussia Dortmund. (the Guardian)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp ndio kizingiti kikuu katika majadiliano yoyote kuhusu usajili wa Philippe Coutinho. (Marca)

Philippe Coutinho hatowasilisha maombi ya kutaka kuondoka Liverpool ili kulazimisha uhamisho wake. (Sport)

West Ham wanajiandaa kutoa dau la pauni milioni 25 kumtaka kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 25. (Daily Mail)

Kiungo wa Chelsea Willian, 29, alizungumza na Manchester United msimu huu kuhusu uwezekano wa kuhamia Old Trafford. (Goal)

Newcastle wamefanikisha usajili wa mkopo wa winga wa Chelsea, Kenedy, 21. (Daily Mirror)

Manchester United wameanza mazungumzo na Zlatan Ibrahimovic, 35, kuhusu mkataba mpya, wakati mchezaji huyo akiendelea kupata nafuu ya jeraha lake la goti. (Daily Mail)

Zlatan Ibrahimovic anaendelea na mazoezi na amemuambia Jose Mourinho kuwa anataka kubakia Old Trafford. (Guardian)

Meneja wa Marseille Rudi Garcia amesema mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud, 30, “atawafaa sana” lakini mfaransa huyo hana mpamgo wa kujiunga na klabu hiyo ya Ligue 1. (L’Equipe)

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez amezungumza na Arsene Wenger wa Arsenal kuhusu kutaka kumsajili Lucas Perez, 28, lakini Arsenal wameshikilia bei ya pauni milioni 13.4. (Chronicle)

Kiungo wa Real Madrid, Isco, 25, anakaribia kusaini mkataba mpya na hivyo kuwanyima nafasi Manchester United na Arsenal ya kumsajili. (Independent)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte ameiambia bodi ya klabu yake kumsajili beki wa kulia wa Barcelona Sergi Roberto, 25. (Sport)

Beki wa Valencia Joao Cancelo, 23, anakaribia kujiunga na Chelsea. (Don Balon)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Wednesday, August 9, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATANO 09.08.2017
Barcelona wanataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, ifikapo mwisho wa wiki hii. (Mirror)

Liverpool wamekataa kumuuza Coutinho licha ya maafisa wa Barcelona kwenda England kujadili uhamisho huo na wapo tayari kuongeza dau lao la pauni milioni 120. (Star)

Rais wa Real Madrid Florentino Perez amewaambia waandishi wa habari kuwa klabu yake haina mpango wa kumuuza Gareth Bale, 28, kufuatia Manchester United kumnyatia. (Star)

Katika mazungumzo ya faragha Florentino Perez amemuambia Jose Mourinho kuwa yuko tayari kumuuza Bale. (Diario Gol)

Meneja wa Chelsea ameitaka klabu yake kupanda dau kumtaka beki wa Tottenham Danny Rose, 27. (Sun)

Chelsea wanataka kumsajili Joao Cancelo kutoka Valencia. (Sky)

Manchester City wamemuulizia kiungo wa Barcelona Sergio Busquets, 29. (Onda Sera)

Inter Milan wamejiunga katika mbio za kutaka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Leicester City Riyad Mahrez, 26, baada ya dau la pauni milioni 32, la Roma kukataliwa. Leicester wanataka pauni milioni 50. (Mirror)

Paris Saint-Germain wapo tayari kuwazidi kete Manchester City kwa kutoa pauni milioni 80 kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28. (Independent)

Kylian Mbappe, 18, ameamua kuwa anataka kwenda Paris Saint-Germain, huku PSG wakijiandaa kutoa euro milioni 155 kumsajili mchezaji huyo wa Monaco. (Telefoot)

Chelsea na Manchester United wamepewa ishara ya kumfuatilia beki wa kulia wa PSG Serge Aurier, 24, baada ya klabu hiyo kusema mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast anauzwa. (Telegraph)

Southampton wako tayari kumuacha Virgil van Dijk “aozee benchi” kuliko kumuuza. (Express)

Mazungumzo ya Everton na Swansea kuhusu usajili wa Gylfi Sigurdsson yameporomoka. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa Leicester City Ahmed Musa, 24, huenda akajiunga na Hull City. (Leicester Mercury)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Tuesday, August 8, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 08.08.2017
Paris Saint-Germain wapo tayari kupanda dau kumtaka mshambuliaji wa Monaco, Kylian Mbappe, 18, na wanajiandaa kutoa pauni milioni 161 kumtaka mchezaji huyo anayesakwa pia na Real Madrid na Manchester City. PSG watamuuza Angel Di Maria ili kupata fedha zaidi za kukamilisha usajili huo. (Le Parisien)

Liverpool watapanda dau la pauni milioni 60 kumtaka Virgil van Dijk kufuatia hatua ya mchezaji huyo kuwasilisha rasmi maombi ya kutaka kuondoka Southampton. Chelsea pia wanamtaka beki huyo, ingawa Antonio Conte anataka zaidi kusajili mabeki wa pembeni huku Serge Aurier wa PSG akiwa miongoni mwao. (Express)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ameghadhibishwa na matatizo ya beki wa PSG Serge Aurier ya kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza, na hivyo kuamua kuelekeza nguvu zake kumtaka Fabinho wa Monaco na anadhani dau la pauni milioni 45 litatosha kumshawishi. (Don Balon)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atakataa mkataba wowote kuhusu Philippe  Coutinho kuondoka Anfield kwenda Barcelona. (Daily Mirror)

Liverpool hawataweza kumzuia Philippe Coutinho, 25, kuondoka msimu huu amesema mkongwe wa klabu hiyo Greame Souness. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa England Ian Wright amesema Philippe Coutinho “hana budi kwenda” Barcelona. (BBC Radio 5 Live)

Barcelona bado wanataka kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20. (Sport)

Manchester United watapanda dau kutaka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale, 28, ikiwa mchezaji huyo ataachwa na Zinedine Zidane katika kikosi kitakachocheza fainali ya Uefa Super Cup. (Times)

Meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane ametupilia mbali taarifa za Gareth Bale kurejea England. (Mirror)

Chelsea na Manchester United zote zitapanda dau kumtaka beki wa PSG Serge Aurier, 24. (Daily Mail)

Kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater anajiandaa kuiambia klabu yake kuwa anataka kuondoka na kujiunga na Chelsea. (Mirror)

Eden Hazard yuko  tayari kuondoka Chelsea na kujiunga na Real Madrid. (Don Balon)

Chelsea wana matumaini makubwa ya kumpata beki wa Southampton Virgil van Dijk kwa sababu ya uhusiano tete kati ya Liverpool na Southampton. (Telegraph)

Southampton wanapanga kumsajili beki wa kati wa Middlesbrough Ben Gibson, 24, kuziba nafasi ya Virgil van Dijk. (Sun)

Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Ian Wright amesema Arsenal walitakiwa kumsajili Nemanja Matic kutoka Chelsea kwa sababu timu hiyo inakosa kiongozi uwanjani. (BBC Radio 5 Live)

Manchester United na Inter Milan zimerejea tena kumtaka beki wa kushoto wa Tottenham Danny Rose, 27. (Daily Mirror)

Manchester City wamemuulizia kiungo wa Barcelona Sergio Busquets. (Onda Cero)

Valencia wanajiandaa kupanda dau la kumshawishi beki wa Arsenal Gabriel, 26, kuhamia Uhispania. (Evening Standard)

Trabzonspor ya Uturuki inataka kumsajili kiungo wa Tottenham Moussa Sissoko, 27, kwa mkopo. (Evening Standard)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Monday, August 7, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU 07.08.2017
Barcelona watawapa Liverpool pauni milioni 120 za kumsajili Philippe Coutinho, 25, baada ya Neymar, 25, kwenda Paris Saint-Germain. (Star)

Licha ya meneja wa Liverpool Jurgen Klopp kusema Philippe Coutinho hauzwi, Barcelona wanazidi kuwa na uhakika wa kukamilisha usajili wiki hii kwa pauni milioni 90. (Sun)

Barcelona wanaweza kutumia fedha walizopata za mauzo ya Neymar kwa kumsajili kiungo mshambuliaji wa PSG Julian Draxler, 23, ambaye wakala wake ameonekana katika mitaa ya Barcelona. (Bild)

Antonio Conte anamtaka beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26, na pia ameitaka bodi ya Chelsea kufanya usajili zaidi baada ya kuona kikosi chake kikifungwa na Arsenal. (Daily Mirror)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp yuko tayari kuacha kumfuatilia Virgil van Dijk, na badala yake kuwaamini mabeki aliokuwa nao sasa. (Mirror)

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema wachezaji zaidi wataondoka Emirates kabla ya dirisha la usajili kufungwa kwa sababu kikosi chake ni kikubwa mno. (Telegraph)

Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, yuko tayari kukubali hali ilivyo- ya Arsenal kugoma kumuuza- na atabakia hadi mkataba wake utakapomalizika na kuondoka bure msimu ujao. (Mirror)

Barcelona wamekubaliana na mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20, lakini sasa wanahitaji kukubaliana ada ya uhamisho ambayo Dortmund wamesema wanataka pauni milioni 90.2. (L’Equipe)

Barcelona wapo kwenye mazungumzo ya kutaka kumsajili kiungo wa zamani wa Tottenham Paulinho, 29, kutoka Guanghzhou Evergrande ya China. (Sport)

Chelsea wapo tayari kupambana na Manchester United katika kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale, 28, ambaye atagharimu takriban pauni milioni 90. (Express)

Chelsea, Manchester United na Monaco zinamtaka beki wa Barcelona Sergi Roberto, 25, ambaye anaweza kuuzwa kwa pauni milioni 36.1. (Don Balon)

Manchester United wamepanda dau la pauni milioni 36 kumtaka Sergi Roberto, lakini Barcelona wamesema mchezaji huyo hauzwi. (Mundo Deportivo)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ameutaka utawala wa klabu yake kumsajili beki wa kulia wa Monaco, Fabinho, 23. (Don Balon)

Baada ya Nemanja Matic kwenda Manchester United kinyume na matakwa yake, meneja wa Chelsea Antonio Conte amekiri kuwa hawezi kuzuia uuzwaji wa Eden Hazard, 26, ambaye ananyatiwa na Barcelona. (Star)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.wakubishiwa.bogspot.com
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Saturday, August 5, 2017

Usajili

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 05.08.2017
Chelsea wameripotiwa kuwasiliana na Paris Saint-Germain kutaka kumsajili beki Serge Aurier, 24, huku kukiwa na taarifa kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast anakaribia kujiunga na Manchester United. (Manchester Evening News)

Inter Milan wanataka kuwapiku Manchester United na Chelsea katika kumsajili beki Serge Aurier wa PSG. (Calciomercato)

Meneja wa Monaco Leonardo Jardim amedokeza kuwa Kylian Mbappe, 18, anayenyatiwa na Real Madrid, Manchester City, Barcelona na Arsenal, huenda akaondoka kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Independent)

Philippe Coutinho, 25, ameachwa katika kikosi cha Liverpool kitakachocheza na Athletic Bilbao siku ya Jumamosi kwa sababu ya jeraha la mgongo. Mchezaji huyo ananyatiwa na Barcelona ili kuziba nafasi ya Neymar. (Mirror)

Barcelona wamewasiliana na Borussia Dortmund kuhusu mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Ousmane Dembele, 20, ili kuchukua nafasi ya Neymar. (Daily Mail)

Ousmane Dembele amesema anakaribisha taarifa za yeye kuhusishwa na kuhamia Barcelona. (Metro)

Barcelona nao wamejiunga katika mbio za kutaka kumsajili winga wa Monaco Thomas Lemar anayenyatiwa na Arsenal. (L’Equipe)

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, 32, amekiri kuwa angependa kurejea England, wakati akizungumza mahakamani kwenye kesi yake ya tuhuma za kukwepa kodi nchini Uhispania. (Cadena SER)

Real Madrid watafikiria kumuuza winga Gareth Bale, 28, kwenda Manchester United, lakini ikiwa tu kipa David De Gea atahusishwa katika mkataba huo. (Don Balon)

Gareth Bale amemuambia mchezaji mwenzake Luka Modric kuwa anataka kurejea England na kujiunga na Manchester United. (Don Balon)

Paris Saint-Germain baada ya kumsajili Neymar, sasa wanataka kupambana na Arsenal katika kumsajili kiungo wa Nice Jean Michael Seri, 26. (Metro)

Monaco wapo tayari kupanda dau la pauni milioni 45 kumtaka mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28. (Sun)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte imeripotiwa yuko tayari kumruhusu beki Andreas Christensen, 21, kwenda Inter Milan ili kubadilishana na winga Antonio Candreva, 30. (Tuttosport)
Kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater yuko tayari kuiambia klabu yake kuwa anataka kuondoka na kujiunga na Chelsea. (Mirror)

Chelsea wamekanusha habari kuwa Antonio Conte anamtoa kwa nguvu Diego Costa, 28, Stamford Bridge. (Independent)

AC Milan wanafikiria kumchukua mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na Chelsea Radamel Falcao, 31. (Sky Sport Italia)

Kiungo wa Inter Milan Geoffrey Kongodbia, 26, anayesakwa na Liverpool na Tottenham, ameomba kuondoka katika klabu yake. (Gazzetta dello Sport)

Everton huenda wakalipa pauni milioni 50 ambayo itavunja rekodi ya klabu ili kumsajili kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27. (The Times)

Watford wanamtaka beki wa Liverpool Alberto Moreno, 25, baada ya Liverpool kukataa dau la pauni milioni 11 kutoka Napoli. (Liverpool Echo)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumamosi njema.

Thursday, August 3, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 03.08.2017
Neymar Jr, 25, atavaa jezi namba 10 atakapokamilisha uhamisho wake kutoka Barcelona kwenda Paris Saint-Germain. (The Mirror)

Mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, ameamua kuondoka katika klabu hiyo huku Real Madrid, Manchester City na Paris Saint-Germain zikipambana kumsajili. (L’Equipe)

Barcelona tayari wamewasiliana na Monaco kuhusu Kylian Mbappe. (Le10Sport)

Ligi ya Uhispania haitokubali kupokea malipo ya kutengua kifungu cha uhamisho cha Neymar kutoka PSG kwa sababu ya mzozo wa malipo ya uzalendo kati ya Neymar na Barca na pia wasiwasi kuhusu PSG kukiuka kanuni za fedha za UEFA. (Sport)

UEFA itaitaka PSG kujieleza jinsi inavyopanga kupata fedha za usajili wa Neymar. (Daily Telegraph)

Barcelona hawatojaribu kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Antoinne Griezmann, 26, licha ya Neymar kuonekana kuwa anaondoka. (AS)

Barcelona wataziba pengo la Neymar kwa kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Ousmane Dembele, 20, anayechezea Borussia Dortmund. (Marca)

Borussia Dortmund wamekataa dau la Arsenal la kumtaka Ousmane Dembele, 20. (Mundo Deportivo)
Wakala wa zamani wa Neymar Wagner Ribeiro amesema “PSG watalipa kitita cha kutengua kifungu cha usajili” wa mchezaji huyo wa Brazil na kuwa “Neymar atatambulishwa rasmi kwa mashabiki wiki hii”. (Marca)

Barcelona watatumia fedha za mauzo ya Neymar kwa kumsajili kiungo mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, 26, na Philippe Coutinho wa Liverpool. (Daily Mail)

Manchester United wapo tayari kumpa nafasi katika kikosi cha kwanza kiungo chipukizi Scott McTominay, 20. (Daily Record)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema atakuwa “mwenye furaha” iwapo timu yake itaweza kusajili mchezaji mwingine tena. (Daily Express)

Jose Mourinho amesema mshambuliaji Anthony Martial, 21, haondoki Manchester United licha ya kuhusishwa na kuhamia Inter Milan. (Daily Star)

Meneja wa Man Utd Jose Mourinho angependa kusajili wachezaji wengine watatu kabla ya dirisha la usajili kufungwa, hata hivyo United inaarifiwa wamekata tamaa ya kumsajili winga wa Inter Milan, Ivan Perisic. (Daily Express)

Meneja wa Tottenham anataka kumfanya kipa Paulo Gazzaniga, 25, kuwa usajili wake wa kwanza kwa kutoa pauni milioni 2 kwa Southampton. (Sun)

Meneja wa Atletico Madrid Diego Simione ameiambia bodi ya klabu yake kuwa lazima wamsajili Diego Costa, 28, ambaye Chelsea wanasema anauzwa kwa pauni milioni 50. (Evening Standard)

Chelsea hawana haraka ya kumuuza Diego Costa, na wamedhamiria kushikilia bei ya pauni milioni 50. (Daily Star)

Chelsea wanatazamia kumsajili kiungo wa Leicester Danny Drinkwater, 27, badala ya Renato Sanches, 19 wa Bayern Munich. (Mediaset)

Uhamisho wa pauni milioni 50 wa kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, kutoka Swansea kwenda Everton unatarajiwa kukamilika siku chache zijazo. (Guardian)

Beki wa Southampton anayenyatiwa na Liverpool Virgil van Dijk, 26, anakaribia kulazimisha uhamisho wake. (daily Mirror)

Kiungo anayesakwa na Liverpool Naby Keita, 22, huenda akakataa kusaini mkataba mpya RB Leipzig. (Bild)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema

Tuesday, August 1, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 01.08.2017
Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa, 28, hatojiunga na kikosi cha kwanza kwa ajili ya kuanza mazoezi siku ya Jumanne huku akiendelea kufuatilia uhamisho wake kuondoka Stamford Bridge. (Marca)

Meneja wa Juventus Massimiliano Allegri ameiambia Chelsea kuwa hawatomuuza beki wa kushoto Alex Sandro, 26. (Sport Mediaset)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte anataka kumsajili kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater, 27, baada ya Nemanja Matic kwenda Man Utd. (Mail)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp huenda akaamua kumfuatilia kiungo wa Bayern Munich Renato Sanches, 19, iwapo Philippe Coutinho, 25, ataondoka kwenda Barcelona. (Bild)

Bayern Munich wamekataa dau la pauni milioni 10 kutoka kwa AC Milan wanaomtaka Renato Sanches, 19, kwa mkopo. (Le10Sport)

Beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26, atakuwa na mazungumzo na meneja wake mpya Mauricio Pellegrino, wiki hii, huku Liverpool wakijiandaa kuvunja rekodi yao ya usajili kumchukua beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi. (Liverpool Echo)

Liverpool wamekataa kukata tamaa katika kumfuatilia beki wa Southampton Virgil van Dijk na watajaribu tena kufanikisha usajili huo kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Daily Mail)

Dau la euro milioni 100 kutoka kwa Barcelona kumtaka Philippe Coutinho, 25, limekataliwa na Liverpool. Barca walipanda dau jingine baada ya euro milioni 80 za awali pia kutupiliwa mbali huku Liverpool wakisisitiza kuwa mchezaji huyo hauzwi. (RMCSport)

Liverpool wanamnyatia kiungo wa Monaco anayesakwa pia na Arsenal, Thomas Lemar, 21. (Le 10Sport)

Inter Milan wanapanga kutoa dau la pauni milioni 35 kumtaka winga wa Liverpool Sadio Mane. (Daily Express)

Inter Milan huenda wakawazidi kete Arsenal katika kumsajili beki wa Nice, Dalbert, 23, kwa pauni milioni 17. (TMW)

Tottenham na Inter Milan zinafikiria kwanza kabla ya kutaka kumsajili beki wa Paris Saint-Germain Serge Aurier, 24, wakiwa na matumaini kuwa ada yake ya uhamisho itapunguzwa. (La Parisien)

Manchester United wamefikia makubaliano na beki wa kulia Serge Aurier, 24, wa PSG, lakini atalazimika kwanza kwenda mahakamani ili kupewa ruhusa ya kuingia Uingereza. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alikutwa na hatia ya kumpiga polisi. (The Mirror)

Newcastle wanamtaka mshambuliaji Lucas Perez, 28, wa Arsenal, lakini hawapo tayari kutoa pauni milioni 13.4 wanazotaka Arsenal. (London Evening Standard)

Calgiari, Sassuolo na Verona za Italia zote zinamtaka beki wa Arsenal Carl Jenkinson, 25. (Corriere dello Sport)

Everton wataongeza bidii katika kutaka kumsajili kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, kwa kutoa pauni milioni 50 pamoja na beki Callum Connolly, 19. (Wales Online)

Wachezaji kadhaa wa Barcelona ‘wamechoshwa mno’ na sakata linaloendelea kuhusu uhamisho ambao huenda ukavuja rekodi ya dunia wa Neymar kwenda PSG, huku wengine wakiwa wamekata tamaa licha ya kumshawishi mchezaji huyo asiondoke. (SPORT)

Watford wanatarajia kukamilisha usajili wa Richardlison, 20, kutoka Fluminese katika siku chache zijazo baada ya mchezaji huyo kutoka Brazil kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza. (Hertfordshire Mercury)

Newcaste huenda wakamkosa kiungo wa Benfica Andreas Samaris, 28, mwenye thamani ya pauni milioni 17.5. (Mirror)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.