Thursday, August 17, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 18.08.2017
Manchester United wanataka kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar. (Daily Record)

Manchester United bado wana matumaini ya kukamilisha usajili wa Ivan Perisic. (Mirror)

Tottenham wamefikia makubaliano ya kimsingi ya kumsajili Davinson Sanchez, 21, kutoka Ajax kwa pauni milioni 28 na milioni 14 zaidi kama marupurupu. (Independent)

Manchester City wapo tayari kuwapa West Brom pauni milioni 22 ili kumsajili nahodha wao Jonny Evans, 29, baada ya dau la pauni milioni 18 kukataliwa, na watampa mara mbili ya mshahara wa pauni 75,000 kwa wiki anaolipwa sasa. (Mirror)

Dau la Chelsea la pauni milioni 62 kumtaka beki wa Juventus Alex Sandro, limekataliwa. (Mirror)

Chelsea wanajiandaa kumuuza Diego Costa kwa hasara. (Sun)

Mkurugenzi wa michezo wa Barcelona Robert Fernandez amesema itakuwa “vigumu” kumsajili kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, kwa sababu hana kipengele cha uhamisho kwenye mkataba wake. (Liverpool Echo)

Barcelona “watapigana” mpaka siku ya mwisho ya usajili ili kumsajili Philippe Coutinho kutoka Liverpool. (Telegraph)
Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa, 28, amesema hatorudi Stamford Bridge na anataka kujiunga na Atletico Madrid. (Telegraph)

Everton huenda wakamtaka Diego Costa kwa mkopo. (Sun)

Beki wa Tottenham Kevin Wimmer, 24, anazungumza na Stoke City kuhusu uhamisho wake wa pauni milioni 15. (Telegraph)

Stoke City pia wanataka kumsajili Kevin Wimmer kutoka Spurs. (Stoke Sentinel)

Beki wa Arsenal Gabriel, 26, anakaribia kujiunga na Valencia kwa pauni milioni 10. (Evening Standard)

Paris Saint-Germain bado wanataka kumsajili kiungo mkabaji wa Monaco, Fabinho, 23. (L’Equipe)

Kiungo wa PSG Blaise Matuidi, 30, amekamilisha vipimo vya afya Juventus, lakini timu hizo mbili bado hazijakubaliana jinsi ada ya uhamisho itakavyolipwa, huku meneja wa PSG Unai Emery akisema hakutaka kumuuza mchezaji huyo. (Le Parisien)

Wakurugenzi wa Borussia Dortmund wamesema Barcelona “hata hawapo karibu” katika kufikia dau la mshambuliaji wake Ousmane Dembele, 20. (Kicker)

Fiorentina wamemwambia mshambuliaji wake Nikola Kalinic, 29, anayenyatiwa na AC Milan kuwa atapigwa faini kwa kutotokea mazoezini siku ya Alhamisi. (Sun)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumaa Kareem.

Monday, August 14, 2017

Tetesi za soka ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU 14.08.2017
Chelsea wanafikiria kutaka kumsajili mchezaji anayenyatiwa na Manchester United Ivan Perisic , 28, kutoka Inter Milan. (Mirror)

Barcelona wanataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, 26. (Diario Gol)

Cezar Azpilicueta, 27, anadhani Chelsea wanahitaji kusajili wachezaji kadhaa zaidi kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Evening Standard)

Chelsea wapo tayari kupanda dau la pauni milioni 50 wiki hii kumtaka beki wa kati wa Southampton Virgil van Dijk na kuwapiku Liverpool. (Daily Star)

Manchester United watakuwa tayari kulipa pauni milioni 36.5 kumsajili kiungo wa Barcelona Sergi Roberto, 25, ikiwa mchezaji huyo atataka kuondoka Uhispania. (Don Balon)

Manchester United wanakaribia kufikia makubaliano na Oliveirense ya Ureno kumsajili mshambuliaji Bruno Amorim, 19. (Daily Mail)

Antoinne Griezmann, 26, atachukizwa na hatua ya Atletico Madrid kumuuza kipa wake Jan Oblak na huenda akafikiria kuhamia Manchester United. (Don Ballon)

Leicester City watakataa dau la Roma la pauni milioni 31 la kumtaka Rirad Mahrez. Leicester wanataka pauni milioni 50. (Mirror)

Mkurugenzi mkuu wa Juventus Beppe Marotta amesema wanamtaka kiungo anayesakwa na Liverpool Naby Keita, 22, anayechezea RB Leipzig. (La Gazzetta dello Sport)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema anahitaji kuimarisha kikosi chake kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Liverpool Echo)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anafikiria kumsajili mshambuliaji wa Napoli Lorenzo Insigne, kuchukua nafasi ya Philippe Coutinho anayenyatiwa na Barcelona. (Express)

Barcelona hawatokata tamaa ya kumsajili Philippe Coutinho, 25, kutoka Liverpool, na wapo tayari kutoa pauni milioni 137 kumshawishi mchezaji huyo. (The Sun)

Mshambuliaji wa Real Madrid Marco Asensio atakuwa na mazungumzo ya dharura na klabu yake kuhusiana na kutaka kuhamia Arsenal. (The Mirror)

Tottenham wataongeza bidii ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Lazio Keita Balde, 22, ambaye hakupangwa katika kikosi cha kwanza kwenye mechi iliyopita. (Mirror)

Winga wa PSG Jese Rodriguez, 24, amekataa kwenda Fiorentina kwa mkopo na anajiandaa kwenda Stoke kwa mkopo. (Sun)

Schalke wanazungumza na Chelsea kuhusu kumchukua tena kwa mkopo beki Baba Rahman, 23. (Sky Sports)

Newcastle wameongeza bidii ya kujaribu kumsajili kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25, baada ya mchezaji huyo kuachwa katika kikosi kilichocheza dhidi ya Leicester. (Sun)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.

Sunday, August 13, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 13.08.2017
Paris Saint-Germain wamekamilisha usajili wa Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco kwa pauni milioni 173. (The Times)

Real Madrid watawapiku Barcelona katika kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20. (RAC-1)

Manchester United wametupilia mbali dau la Tottenham la kumtaka Anthony Martial, 21. (RMC Sport)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atataka kumsajili mshambuliaji wa Napoli Lorenzo Insigne, 26, iwapo Philippe Coutinho, 25, atalazimisha kuondoka na kwenda Barcelona. (Sunday People)

Barcelona watarejea Liverpool na dau la pauni milioni 100 kumtaka Philippe Coutinho. (Sunday Express)

Chelsea wiki hii watapanda dau la pili la takriban pauni milioni 25 kumtaka kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater, 27, baada ya pauni milioni 15 za awali kukataliwa. (Sunday Telegraph)

Real Madrid wamekiri kukata tamaa ya kutaka kumsajili kipa wa Manchester United David De Gea msimu huu. (Sunday Express)

Barcelona wamemsajili kiungo wa zamani wa Tottenham, Paulinho, 29, kwa pauni milioni 36.6 kutoka Guangzhou Evergrande ya China. (Mail on Sunday)

Paris Saint-Germain huenda wakatumia zaidi ya pauni milioni 54.9 kumsajili beki wa Monaco Fabinho, 23. (ESPN)

Kiungo Mjerumani Mesut Ozil, 28, hataki kubakia Arsenal na anataka kulazimisha uhamisho wa kwenda Barcelona. (Don Balon)

Tottenham watamwaga fedha kabla ya dirisha la usajili kufungwa, wakianza na kupanda dau la kumtaka kiungo wa Everton Ross Barkley, 23. (Sunday Telegraph)

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anahoji kwanini wanamfuatilia Ross Barkley, yeye anawataka zaidi kiungo wa Celta Vigo Pape Cheikh Diop, 20, na beki wa Ajax Davinson Sanchez, 21. (Sun on Sunday)

Ajax wamekataa dau la pauni milioni 36.6 kutoka Tottenham la kumtaka Davinson Sanchez, na amepewa mkataba mpya ili kumshawishi asalie Ajax. (De Telegraaf)

Chelsea watakuwa tayari kumuuza Eden Hazard, 26, iwapo Barcelona watakuwa tayari kutoa pauni milioni 110. (Diario Gol)

Manchester United wameanza tena mazungumzo na Inter Milan ya kutaka kumsajili winga Ivan Perisic, 28, na wanakaribia kutoa kitita cha pauni milioni 48 wanachotaka Inter. (Sunday Mirror)

Chelsea wana wasiwasi kuwa mshambuliaji wake Diego Costa, 28, amenenepa sana baada ya kwenda likizo ya mapumziko Brazil na huenda ikawa vigumu kumuuza. (Sunday Times)

Diego Costa huenda akapigwa faini na Chelsea kwa kushindwa kurejea mazoezini wiki mbili zilizopita. (Daily Star)

Liverpool wamemuambia Emre Can, 23, kuwa haendi popote licha ya Juventus kujipanga kutoa pauni milioni 23 kumtaka kiungo huyo Mjerumani ambaye amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake. (Sunday Mirror)

Kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, hatimaye atakamilisha uhamisho wake kwenda Everton wiki hii, na hivyo kufanya Swansea kumfuatilia kiungo wa West Brom Nacer Chadli, 28, na huenda kusababisha Tottenham kumsajili Ross Barkley, 23, kutoka Everton. (Sunday People)

Meneja wa Everton Ronald Koeman, baada ya kumsajili Gylfi Sigurdsson atataka kumsajili mshambuliaji wa Fiorentina Nikola Kalinic, 29. (Sunday Express)

Mshambuliaji wa kimataifa wa Croatia na Fiorentina Nikola Kalinic, 29, anataka kwenda AC Milan. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Antoinne Griezmann, 26, huenda akaondoka Atletico Madrid, iwapo kipa Jan Oblak, 24, atauzwa kwenda PSG. (Don Balon)

Kiungo mshambuliaji wa Real Madrid Marco Asensio, 21, anataka kutumia nafasi ya Arsenal kumnyatia ili apate mkataba mpya Real. (Diario Balon)

Arsenal wamekata tamaa ya kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar, 21, na sasa meneja Arsene Wenger anatazama zaidi kupunguza wachezaji asiowahitaji ili kupunguza gharama za mishahara. (Mail on Sunday)

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez anataka kumsajili kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25. (Sun on Sunday)

Tukutane baadaye katika BBC Ulimwengu wa Soka ambapo tutakutangazia mechi ya Manchester United v West Ham United.

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumapili njema.

Friday, August 11, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 11.08.2017
Arsenal wamempa Alexis Sanchez mkataba mpya na mshahara wa pauni 300,000 kwa wiki na kumfanya mchezaji anayelipwa zaidi katika EPL. (Daily Mail)

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekiri kuwa “hana uhakika sana” kama ataweza kumshawishi Alexis Sanchez kukubali kusaini mkataba mpya. (SFR)

Juventus wanajiandaa kutoa pauni milioni 23 kujaribu kuishawishi Liverpool kumuuza Emre Can. (Gazzetta dello Sport)

Juventus nao wameingia katika mbio za kutaka kumsajili Sergi Roberto kutoka Barcelona, ambaye pia Manchester United na Chelsea zinamtaka. (Sport.es)

West Ham wamepanda dau la pauni milioni 27.1 kumtaka kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 25. (Daily Telegraph)

Barcelona hawatakuwa na uwezo wa kumnunua Philippe Coutinho kutoka Liverpool iwapo watafanikiwa kumsajili Ousmane Dembele, 20, kutoka Borussia Dortmund, kwa mujibu wa mwandishi wa ha1ba12ri za michezo Graham Hunter. (BBC Radio 5 Live)

Barcelona wapo tayari kuwapa Liverpool Ivan Rakitic kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Philippe Coutinho. (Don Balon)

Barcelona wanamtaka kiungo mchezeshaji wa Real Madrid Marco Asensio na wapo tayari kutoa pauni milioni 72. (Diario Gol)

Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Lexy anakabiliwa na sekeseke la wachezaji kudai kuongezewa mishahara baada ya beki Danny Rose kushutumu sera za klabu hiyo. (Daily Mirror)

Danny Rose alipokelewa kwa shangwe na wachezaji wenzake baada ya kuweka wazi mtazamo wa Tottenham, huku wachezaji wengine wakitishia na wao kuweka mambo hadharani. (Daily Mirror)

Wachezaji nyota wa Tottenham wanataka kuondoka kwa sababu ya sera ya malipo ya klabu hiyo. (Daily Mail)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anatafuta beki wa kushoto na Danny Rose wa Tottenham ni mmoja wa wachezaji anaowafuatilia. (Daily Record)

Meneja wa Everton Ronald Koeman ameiambia Tottenham kuwa hawataweza kumsajili kiungo Ross Barkley kwa bei rahisi. (Daily Star)

Arsenal wanaamini kuwa wamefanikiwa katika mazungumzo ya kumshawishi Mesut Ozil kubakia Emirates baada ya kumpa mkataba wa mshahara wa pauni 225,000 kwa wiki, na mchezaji huyo ameonesha dalili za kukubali. (Sun)
PSG wapo tayari kuwapa Atletico Madrid Javier Pastore katika mkataba wa kumsajili kipa Jan Oblak, 24. (AS)

Real Madrid wamekuwa na mazungumzo ya siri na Juventus kuhusiana na mshambuliaji Paulo Dybala, 23, ambaye pia anasakwa na Barcelona. (Don Balon)

Juventus wanamtaka Kevin Strootman kabla ya dirisha la usajili kufungwa, huku Roma wakisema bei yake ni euro milioni 45. (Tuttosport)

Arsene Wenger amesema meneja wa Chelsea Antonio Conte awarejeshe wachezaji wanaocheza nje kwa mkopo kama ana wasiwasi na idogo wa kikosi chake. (Times)

Msimu wa EPL unaanza rasmi leo. Arsenal wanacheza na Leicester City saa nne kasorobo usiku huu kwenye uwanja wa Emirates. Matokeo ya mchezo huo utayapata hapa hapa.

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumaa Kareem.

Thursday, August 10, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 10.08.2017
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anataka kusajili angalau mchezaji mmoja zaidi kabla ya dirisha la usajili kufungwa, huku beki wa kushoto Danny Rose, 27, na winga wa Inter Milan Ivan Perisic wakiendelea kunyatiwa na United. (Manchester Evening News)

Jose Mourinho ameitaka Manchester United kupanda dau la pauni milioni 100 kumtaka Gareth Bale wa Real Madrid. (The Sun)

Danny Rose amesema hana mpango wa kuondoka Tottenham, lakini anaamini anastahili kulipwa zaidi kuliko anavyolipwa sasa. (Sun)

Danny Rose ameitaka Tottenham kusajili wachezaji wenye majina makubwa. (Sun)

Tottenham wapo tayari kutoa pauni milioni 55 kumtaka beki wa Ajax Davinson Sanchez. (The Sun)

Paris Saint-Germain wanakaribia kumsajili mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, kwa pauni milioni 163, na tayari wamekamilisha mkataba na Fabinho, 23, pia wa Monaco. (Daily Record)

Iwapo Kylian Mbappe ataondoka, Monaco wataamua kumfuatilia mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia, Carlos Bacca anayeichezea AC Milan. (Caracol Radio)

Chelsea wamepanda dau la pauni milioni 35 kumtaka kiungo mshambuliaji wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Daily Star)

Chelsea wanazidi kuonekana kuwa na nafasi zaidi ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Everton Ross Barlkey, ambaye pia ananyatiwa na Tottenham. (Daily Telegraph)

Arsenal wana wasiwasi kuwa mshambuliaji wake Alexis Sanchez, 28, huenda akataka kulazimisha uhamisho wake kuondoka Emirates. (Daily Mirror)

Barcelona watarejea tena Liverpool na dau la nne la kumtaka kiungo mshambuliaji kutoka Brazil Philippe Coutinho, 25. (Daily Mail)

Barcelona na Atletico Madrid wanapambana katika kutaka kumsajili Lautaro Martinez anayechezea Racing Club ya Argentina. (El Grafico)

Barcelona wameambiwa walipe pauni milioni 135 kama wanataka kumsajili Ousmane Dembele, 20, wa Borussia Dortmund. (the Guardian)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp ndio kizingiti kikuu katika majadiliano yoyote kuhusu usajili wa Philippe Coutinho. (Marca)

Philippe Coutinho hatowasilisha maombi ya kutaka kuondoka Liverpool ili kulazimisha uhamisho wake. (Sport)

West Ham wanajiandaa kutoa dau la pauni milioni 25 kumtaka kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 25. (Daily Mail)

Kiungo wa Chelsea Willian, 29, alizungumza na Manchester United msimu huu kuhusu uwezekano wa kuhamia Old Trafford. (Goal)

Newcastle wamefanikisha usajili wa mkopo wa winga wa Chelsea, Kenedy, 21. (Daily Mirror)

Manchester United wameanza mazungumzo na Zlatan Ibrahimovic, 35, kuhusu mkataba mpya, wakati mchezaji huyo akiendelea kupata nafuu ya jeraha lake la goti. (Daily Mail)

Zlatan Ibrahimovic anaendelea na mazoezi na amemuambia Jose Mourinho kuwa anataka kubakia Old Trafford. (Guardian)

Meneja wa Marseille Rudi Garcia amesema mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud, 30, “atawafaa sana” lakini mfaransa huyo hana mpamgo wa kujiunga na klabu hiyo ya Ligue 1. (L’Equipe)

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez amezungumza na Arsene Wenger wa Arsenal kuhusu kutaka kumsajili Lucas Perez, 28, lakini Arsenal wameshikilia bei ya pauni milioni 13.4. (Chronicle)

Kiungo wa Real Madrid, Isco, 25, anakaribia kusaini mkataba mpya na hivyo kuwanyima nafasi Manchester United na Arsenal ya kumsajili. (Independent)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte ameiambia bodi ya klabu yake kumsajili beki wa kulia wa Barcelona Sergi Roberto, 25. (Sport)

Beki wa Valencia Joao Cancelo, 23, anakaribia kujiunga na Chelsea. (Don Balon)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Wednesday, August 9, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATANO 09.08.2017
Barcelona wanataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, ifikapo mwisho wa wiki hii. (Mirror)

Liverpool wamekataa kumuuza Coutinho licha ya maafisa wa Barcelona kwenda England kujadili uhamisho huo na wapo tayari kuongeza dau lao la pauni milioni 120. (Star)

Rais wa Real Madrid Florentino Perez amewaambia waandishi wa habari kuwa klabu yake haina mpango wa kumuuza Gareth Bale, 28, kufuatia Manchester United kumnyatia. (Star)

Katika mazungumzo ya faragha Florentino Perez amemuambia Jose Mourinho kuwa yuko tayari kumuuza Bale. (Diario Gol)

Meneja wa Chelsea ameitaka klabu yake kupanda dau kumtaka beki wa Tottenham Danny Rose, 27. (Sun)

Chelsea wanataka kumsajili Joao Cancelo kutoka Valencia. (Sky)

Manchester City wamemuulizia kiungo wa Barcelona Sergio Busquets, 29. (Onda Sera)

Inter Milan wamejiunga katika mbio za kutaka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Leicester City Riyad Mahrez, 26, baada ya dau la pauni milioni 32, la Roma kukataliwa. Leicester wanataka pauni milioni 50. (Mirror)

Paris Saint-Germain wapo tayari kuwazidi kete Manchester City kwa kutoa pauni milioni 80 kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28. (Independent)

Kylian Mbappe, 18, ameamua kuwa anataka kwenda Paris Saint-Germain, huku PSG wakijiandaa kutoa euro milioni 155 kumsajili mchezaji huyo wa Monaco. (Telefoot)

Chelsea na Manchester United wamepewa ishara ya kumfuatilia beki wa kulia wa PSG Serge Aurier, 24, baada ya klabu hiyo kusema mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast anauzwa. (Telegraph)

Southampton wako tayari kumuacha Virgil van Dijk “aozee benchi” kuliko kumuuza. (Express)

Mazungumzo ya Everton na Swansea kuhusu usajili wa Gylfi Sigurdsson yameporomoka. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa Leicester City Ahmed Musa, 24, huenda akajiunga na Hull City. (Leicester Mercury)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Tuesday, August 8, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 08.08.2017
Paris Saint-Germain wapo tayari kupanda dau kumtaka mshambuliaji wa Monaco, Kylian Mbappe, 18, na wanajiandaa kutoa pauni milioni 161 kumtaka mchezaji huyo anayesakwa pia na Real Madrid na Manchester City. PSG watamuuza Angel Di Maria ili kupata fedha zaidi za kukamilisha usajili huo. (Le Parisien)

Liverpool watapanda dau la pauni milioni 60 kumtaka Virgil van Dijk kufuatia hatua ya mchezaji huyo kuwasilisha rasmi maombi ya kutaka kuondoka Southampton. Chelsea pia wanamtaka beki huyo, ingawa Antonio Conte anataka zaidi kusajili mabeki wa pembeni huku Serge Aurier wa PSG akiwa miongoni mwao. (Express)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ameghadhibishwa na matatizo ya beki wa PSG Serge Aurier ya kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza, na hivyo kuamua kuelekeza nguvu zake kumtaka Fabinho wa Monaco na anadhani dau la pauni milioni 45 litatosha kumshawishi. (Don Balon)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atakataa mkataba wowote kuhusu Philippe  Coutinho kuondoka Anfield kwenda Barcelona. (Daily Mirror)

Liverpool hawataweza kumzuia Philippe Coutinho, 25, kuondoka msimu huu amesema mkongwe wa klabu hiyo Greame Souness. (Sky Sports)

Mshambuliaji wa zamani wa kimataifa wa England Ian Wright amesema Philippe Coutinho “hana budi kwenda” Barcelona. (BBC Radio 5 Live)

Barcelona bado wanataka kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20. (Sport)

Manchester United watapanda dau kutaka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale, 28, ikiwa mchezaji huyo ataachwa na Zinedine Zidane katika kikosi kitakachocheza fainali ya Uefa Super Cup. (Times)

Meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane ametupilia mbali taarifa za Gareth Bale kurejea England. (Mirror)

Chelsea na Manchester United zote zitapanda dau kumtaka beki wa PSG Serge Aurier, 24. (Daily Mail)

Kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater anajiandaa kuiambia klabu yake kuwa anataka kuondoka na kujiunga na Chelsea. (Mirror)

Eden Hazard yuko  tayari kuondoka Chelsea na kujiunga na Real Madrid. (Don Balon)

Chelsea wana matumaini makubwa ya kumpata beki wa Southampton Virgil van Dijk kwa sababu ya uhusiano tete kati ya Liverpool na Southampton. (Telegraph)

Southampton wanapanga kumsajili beki wa kati wa Middlesbrough Ben Gibson, 24, kuziba nafasi ya Virgil van Dijk. (Sun)

Mshambuliaji wa zamani wa Arsenal, Ian Wright amesema Arsenal walitakiwa kumsajili Nemanja Matic kutoka Chelsea kwa sababu timu hiyo inakosa kiongozi uwanjani. (BBC Radio 5 Live)

Manchester United na Inter Milan zimerejea tena kumtaka beki wa kushoto wa Tottenham Danny Rose, 27. (Daily Mirror)

Manchester City wamemuulizia kiungo wa Barcelona Sergio Busquets. (Onda Cero)

Valencia wanajiandaa kupanda dau la kumshawishi beki wa Arsenal Gabriel, 26, kuhamia Uhispania. (Evening Standard)

Trabzonspor ya Uturuki inataka kumsajili kiungo wa Tottenham Moussa Sissoko, 27, kwa mkopo. (Evening Standard)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Monday, August 7, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU 07.08.2017
Barcelona watawapa Liverpool pauni milioni 120 za kumsajili Philippe Coutinho, 25, baada ya Neymar, 25, kwenda Paris Saint-Germain. (Star)

Licha ya meneja wa Liverpool Jurgen Klopp kusema Philippe Coutinho hauzwi, Barcelona wanazidi kuwa na uhakika wa kukamilisha usajili wiki hii kwa pauni milioni 90. (Sun)

Barcelona wanaweza kutumia fedha walizopata za mauzo ya Neymar kwa kumsajili kiungo mshambuliaji wa PSG Julian Draxler, 23, ambaye wakala wake ameonekana katika mitaa ya Barcelona. (Bild)

Antonio Conte anamtaka beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26, na pia ameitaka bodi ya Chelsea kufanya usajili zaidi baada ya kuona kikosi chake kikifungwa na Arsenal. (Daily Mirror)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp yuko tayari kuacha kumfuatilia Virgil van Dijk, na badala yake kuwaamini mabeki aliokuwa nao sasa. (Mirror)

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amesema wachezaji zaidi wataondoka Emirates kabla ya dirisha la usajili kufungwa kwa sababu kikosi chake ni kikubwa mno. (Telegraph)

Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, yuko tayari kukubali hali ilivyo- ya Arsenal kugoma kumuuza- na atabakia hadi mkataba wake utakapomalizika na kuondoka bure msimu ujao. (Mirror)

Barcelona wamekubaliana na mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20, lakini sasa wanahitaji kukubaliana ada ya uhamisho ambayo Dortmund wamesema wanataka pauni milioni 90.2. (L’Equipe)

Barcelona wapo kwenye mazungumzo ya kutaka kumsajili kiungo wa zamani wa Tottenham Paulinho, 29, kutoka Guanghzhou Evergrande ya China. (Sport)

Chelsea wapo tayari kupambana na Manchester United katika kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Gareth Bale, 28, ambaye atagharimu takriban pauni milioni 90. (Express)

Chelsea, Manchester United na Monaco zinamtaka beki wa Barcelona Sergi Roberto, 25, ambaye anaweza kuuzwa kwa pauni milioni 36.1. (Don Balon)

Manchester United wamepanda dau la pauni milioni 36 kumtaka Sergi Roberto, lakini Barcelona wamesema mchezaji huyo hauzwi. (Mundo Deportivo)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ameutaka utawala wa klabu yake kumsajili beki wa kulia wa Monaco, Fabinho, 23. (Don Balon)

Baada ya Nemanja Matic kwenda Manchester United kinyume na matakwa yake, meneja wa Chelsea Antonio Conte amekiri kuwa hawezi kuzuia uuzwaji wa Eden Hazard, 26, ambaye ananyatiwa na Barcelona. (Star)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.wakubishiwa.bogspot.com
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.

Saturday, August 5, 2017

Usajili

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 05.08.2017
Chelsea wameripotiwa kuwasiliana na Paris Saint-Germain kutaka kumsajili beki Serge Aurier, 24, huku kukiwa na taarifa kuwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast anakaribia kujiunga na Manchester United. (Manchester Evening News)

Inter Milan wanataka kuwapiku Manchester United na Chelsea katika kumsajili beki Serge Aurier wa PSG. (Calciomercato)

Meneja wa Monaco Leonardo Jardim amedokeza kuwa Kylian Mbappe, 18, anayenyatiwa na Real Madrid, Manchester City, Barcelona na Arsenal, huenda akaondoka kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Independent)

Philippe Coutinho, 25, ameachwa katika kikosi cha Liverpool kitakachocheza na Athletic Bilbao siku ya Jumamosi kwa sababu ya jeraha la mgongo. Mchezaji huyo ananyatiwa na Barcelona ili kuziba nafasi ya Neymar. (Mirror)

Barcelona wamewasiliana na Borussia Dortmund kuhusu mchezaji wa kimataifa wa Ufaransa Ousmane Dembele, 20, ili kuchukua nafasi ya Neymar. (Daily Mail)

Ousmane Dembele amesema anakaribisha taarifa za yeye kuhusishwa na kuhamia Barcelona. (Metro)

Barcelona nao wamejiunga katika mbio za kutaka kumsajili winga wa Monaco Thomas Lemar anayenyatiwa na Arsenal. (L’Equipe)

Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo, 32, amekiri kuwa angependa kurejea England, wakati akizungumza mahakamani kwenye kesi yake ya tuhuma za kukwepa kodi nchini Uhispania. (Cadena SER)

Real Madrid watafikiria kumuuza winga Gareth Bale, 28, kwenda Manchester United, lakini ikiwa tu kipa David De Gea atahusishwa katika mkataba huo. (Don Balon)

Gareth Bale amemuambia mchezaji mwenzake Luka Modric kuwa anataka kurejea England na kujiunga na Manchester United. (Don Balon)

Paris Saint-Germain baada ya kumsajili Neymar, sasa wanataka kupambana na Arsenal katika kumsajili kiungo wa Nice Jean Michael Seri, 26. (Metro)

Monaco wapo tayari kupanda dau la pauni milioni 45 kumtaka mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28. (Sun)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte imeripotiwa yuko tayari kumruhusu beki Andreas Christensen, 21, kwenda Inter Milan ili kubadilishana na winga Antonio Candreva, 30. (Tuttosport)
Kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater yuko tayari kuiambia klabu yake kuwa anataka kuondoka na kujiunga na Chelsea. (Mirror)

Chelsea wamekanusha habari kuwa Antonio Conte anamtoa kwa nguvu Diego Costa, 28, Stamford Bridge. (Independent)

AC Milan wanafikiria kumchukua mshambuliaji wa zamani wa Manchester United na Chelsea Radamel Falcao, 31. (Sky Sport Italia)

Kiungo wa Inter Milan Geoffrey Kongodbia, 26, anayesakwa na Liverpool na Tottenham, ameomba kuondoka katika klabu yake. (Gazzetta dello Sport)

Everton huenda wakalipa pauni milioni 50 ambayo itavunja rekodi ya klabu ili kumsajili kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27. (The Times)

Watford wanamtaka beki wa Liverpool Alberto Moreno, 25, baada ya Liverpool kukataa dau la pauni milioni 11 kutoka Napoli. (Liverpool Echo)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumamosi njema.

Thursday, August 3, 2017

Usajili ulaya

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 03.08.2017
Neymar Jr, 25, atavaa jezi namba 10 atakapokamilisha uhamisho wake kutoka Barcelona kwenda Paris Saint-Germain. (The Mirror)

Mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, ameamua kuondoka katika klabu hiyo huku Real Madrid, Manchester City na Paris Saint-Germain zikipambana kumsajili. (L’Equipe)

Barcelona tayari wamewasiliana na Monaco kuhusu Kylian Mbappe. (Le10Sport)

Ligi ya Uhispania haitokubali kupokea malipo ya kutengua kifungu cha uhamisho cha Neymar kutoka PSG kwa sababu ya mzozo wa malipo ya uzalendo kati ya Neymar na Barca na pia wasiwasi kuhusu PSG kukiuka kanuni za fedha za UEFA. (Sport)

UEFA itaitaka PSG kujieleza jinsi inavyopanga kupata fedha za usajili wa Neymar. (Daily Telegraph)

Barcelona hawatojaribu kumsajili mshambuliaji wa Atletico Madrid, Antoinne Griezmann, 26, licha ya Neymar kuonekana kuwa anaondoka. (AS)

Barcelona wataziba pengo la Neymar kwa kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Ousmane Dembele, 20, anayechezea Borussia Dortmund. (Marca)

Borussia Dortmund wamekataa dau la Arsenal la kumtaka Ousmane Dembele, 20. (Mundo Deportivo)
Wakala wa zamani wa Neymar Wagner Ribeiro amesema “PSG watalipa kitita cha kutengua kifungu cha usajili” wa mchezaji huyo wa Brazil na kuwa “Neymar atatambulishwa rasmi kwa mashabiki wiki hii”. (Marca)

Barcelona watatumia fedha za mauzo ya Neymar kwa kumsajili kiungo mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, 26, na Philippe Coutinho wa Liverpool. (Daily Mail)

Manchester United wapo tayari kumpa nafasi katika kikosi cha kwanza kiungo chipukizi Scott McTominay, 20. (Daily Record)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema atakuwa “mwenye furaha” iwapo timu yake itaweza kusajili mchezaji mwingine tena. (Daily Express)

Jose Mourinho amesema mshambuliaji Anthony Martial, 21, haondoki Manchester United licha ya kuhusishwa na kuhamia Inter Milan. (Daily Star)

Meneja wa Man Utd Jose Mourinho angependa kusajili wachezaji wengine watatu kabla ya dirisha la usajili kufungwa, hata hivyo United inaarifiwa wamekata tamaa ya kumsajili winga wa Inter Milan, Ivan Perisic. (Daily Express)

Meneja wa Tottenham anataka kumfanya kipa Paulo Gazzaniga, 25, kuwa usajili wake wa kwanza kwa kutoa pauni milioni 2 kwa Southampton. (Sun)

Meneja wa Atletico Madrid Diego Simione ameiambia bodi ya klabu yake kuwa lazima wamsajili Diego Costa, 28, ambaye Chelsea wanasema anauzwa kwa pauni milioni 50. (Evening Standard)

Chelsea hawana haraka ya kumuuza Diego Costa, na wamedhamiria kushikilia bei ya pauni milioni 50. (Daily Star)

Chelsea wanatazamia kumsajili kiungo wa Leicester Danny Drinkwater, 27, badala ya Renato Sanches, 19 wa Bayern Munich. (Mediaset)

Uhamisho wa pauni milioni 50 wa kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, kutoka Swansea kwenda Everton unatarajiwa kukamilika siku chache zijazo. (Guardian)

Beki wa Southampton anayenyatiwa na Liverpool Virgil van Dijk, 26, anakaribia kulazimisha uhamisho wake. (daily Mirror)

Kiungo anayesakwa na Liverpool Naby Keita, 22, huenda akakataa kusaini mkataba mpya RB Leipzig. (Bild)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema

Tuesday, August 1, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 01.08.2017
Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa, 28, hatojiunga na kikosi cha kwanza kwa ajili ya kuanza mazoezi siku ya Jumanne huku akiendelea kufuatilia uhamisho wake kuondoka Stamford Bridge. (Marca)

Meneja wa Juventus Massimiliano Allegri ameiambia Chelsea kuwa hawatomuuza beki wa kushoto Alex Sandro, 26. (Sport Mediaset)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte anataka kumsajili kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater, 27, baada ya Nemanja Matic kwenda Man Utd. (Mail)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp huenda akaamua kumfuatilia kiungo wa Bayern Munich Renato Sanches, 19, iwapo Philippe Coutinho, 25, ataondoka kwenda Barcelona. (Bild)

Bayern Munich wamekataa dau la pauni milioni 10 kutoka kwa AC Milan wanaomtaka Renato Sanches, 19, kwa mkopo. (Le10Sport)

Beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26, atakuwa na mazungumzo na meneja wake mpya Mauricio Pellegrino, wiki hii, huku Liverpool wakijiandaa kuvunja rekodi yao ya usajili kumchukua beki huyo wa kimataifa wa Uholanzi. (Liverpool Echo)

Liverpool wamekataa kukata tamaa katika kumfuatilia beki wa Southampton Virgil van Dijk na watajaribu tena kufanikisha usajili huo kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Daily Mail)

Dau la euro milioni 100 kutoka kwa Barcelona kumtaka Philippe Coutinho, 25, limekataliwa na Liverpool. Barca walipanda dau jingine baada ya euro milioni 80 za awali pia kutupiliwa mbali huku Liverpool wakisisitiza kuwa mchezaji huyo hauzwi. (RMCSport)

Liverpool wanamnyatia kiungo wa Monaco anayesakwa pia na Arsenal, Thomas Lemar, 21. (Le 10Sport)

Inter Milan wanapanga kutoa dau la pauni milioni 35 kumtaka winga wa Liverpool Sadio Mane. (Daily Express)

Inter Milan huenda wakawazidi kete Arsenal katika kumsajili beki wa Nice, Dalbert, 23, kwa pauni milioni 17. (TMW)

Tottenham na Inter Milan zinafikiria kwanza kabla ya kutaka kumsajili beki wa Paris Saint-Germain Serge Aurier, 24, wakiwa na matumaini kuwa ada yake ya uhamisho itapunguzwa. (La Parisien)

Manchester United wamefikia makubaliano na beki wa kulia Serge Aurier, 24, wa PSG, lakini atalazimika kwanza kwenda mahakamani ili kupewa ruhusa ya kuingia Uingereza. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast alikutwa na hatia ya kumpiga polisi. (The Mirror)

Newcastle wanamtaka mshambuliaji Lucas Perez, 28, wa Arsenal, lakini hawapo tayari kutoa pauni milioni 13.4 wanazotaka Arsenal. (London Evening Standard)

Calgiari, Sassuolo na Verona za Italia zote zinamtaka beki wa Arsenal Carl Jenkinson, 25. (Corriere dello Sport)

Everton wataongeza bidii katika kutaka kumsajili kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, kwa kutoa pauni milioni 50 pamoja na beki Callum Connolly, 19. (Wales Online)

Wachezaji kadhaa wa Barcelona ‘wamechoshwa mno’ na sakata linaloendelea kuhusu uhamisho ambao huenda ukavuja rekodi ya dunia wa Neymar kwenda PSG, huku wengine wakiwa wamekata tamaa licha ya kumshawishi mchezaji huyo asiondoke. (SPORT)

Watford wanatarajia kukamilisha usajili wa Richardlison, 20, kutoka Fluminese katika siku chache zijazo baada ya mchezaji huyo kutoka Brazil kupata kibali cha kufanya kazi Uingereza. (Hertfordshire Mercury)

Newcaste huenda wakamkosa kiungo wa Benfica Andreas Samaris, 28, mwenye thamani ya pauni milioni 17.5. (Mirror)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.

Sunday, July 30, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 30.07.2017
Baba yake Neymar ameiomba PSG kusubiri kuanza mazungumzo rasmi ya uhamisho wa pauni milioni 450 wa mwanae hadi baada ya Julai 31, tarehe ambayo atapata bakshishi yake ya pauni milioni 23.3 kutoka kwa Barcelona ya kumshawishi Neymar kusaini mkataba mpya mwaka jana Oktoba. (Sunday Times)

Barcelona watawashtaki Paris Saint-Germain kwa UEFA kwa kukiuka kanuni za fedha (FFP) iwapo PSG watatoa dau la pauni milioni 197 kutengua kifungu cha usajili cha Neymar. (ESPN)

Iwapo Neymar, 25, ataondoka Barcelona na kujiunga na PSG, Barca huenda wakaamua kumchukua mshambuliaji wa Atletico Madrid Antoinne Griezmann, 26 kuziba pengo. (Marca)

PSG wakikamilisha usajili wa Neymar, watapanda dau la pauni milioni 35 kumtaka mshambuliaji wa Arsenal, Alexis Sanchez, 28 kutoka Arsenal. (Sunday Express)

Philippe Coutinho, 25, atamuomba meneja wa Liverpool Jurgen Klopp kumruhusu ajiunge na Barcelona. Iwapo Coutinho ataondoka, Klopp atataka kumsajili winga wa Borussia Dortmund Christian Pulisic. (Sunday Mirror)

Meneja wa RB Leipzig amesema kiungo Naby Keita, 22,  anayenyatiwa na Liverpool ana asilimia 100 ya kubakia katika klabu hiyo ya Bundesliga. (Observer)

Uhamisho wa kiungo Nemanja Matic, 28, kutoka Chelsea kwenda Manchester United umekwama kutokana na kutofautiana kuhusu malipo ya marupurupu kwa Chelsea katika sehemu ya mkataba huo. (Sun on Sunday)

Manchester United huenda wakakamilisha usajili wa Nemanja Matic, 28, kutoka Chelsea mwishoni mwa wiki ijayo. (Daily Mail)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho atasubiri hadi msimu ujao kutoa pauni milioni 90 kumsajili Gareth Bale, 28, kutoka Real Madrid. (Sunday Express)

Meneja wa Inter Milan Luciano Spalletti “anapinga vikali” hatua ya kuondoka kwa winga Ivan Perisic, 28, ambaye amehusishwa na Manchester United. (Observer)

Manchester United wanakaribia kukamilisha usajili wa pauni milioni 48 wa Ivan Perisic kutoka Inter Milan. (Daily Star)

Kiungo wa Manchester United Marouanne Fellaini, 29, amekubali mkataba wa kujiunga na Galatasaray ya Uturuki. (Ajansspor)

Manchester United wamehusishwa na kumtaka kiungo wa Anderlecht Leander Dendocker, 22, huku mkurugenzi wa klabu hiyo akisema timu ikija na dau la euro milioni 25-35, itakuwa vigumu kukataa. (Het Belang van Limburg)

Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, yuko tayari kuwasilisha maombi ya rasmi ya uhamisho ili kulazimisha uhamisho wake kwenda Manchester City. (Sunday Mirror)

Manchester City wamerejea katika orodha ya UEFA ya timu zinazomulikwa kwa kukiuka kifungu cha fedha (FFP) baada ya kutumia pauni milioni 220 kusajili msimu huu. (Sunday Telegraph)

Kiungo wa Everton Ross Barkley, 23, anawindwa na timu sita za EPL, huku Tottenham na Manchester City wakiongoza mbio za kutaka kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa England. (Daily Star Sunday)

Everton wanafikiria kutoa pauni milioni 9 kumsajili beki wa West ham Winston Reid. (Mail on Sunday)

Chelsea wapo tayari kutoa hadi euro milioni 70 kumsajili Alex Sandro. (Calciomercato)

Mkurugenzi wa michezo wa Roma, Monci, anasema klabu yake sasa inatazama kwingine baada ya dau jingine la kumtaka Riyad Mahrez, 26, kukataliwa na Leicester. (Evening Standard)

Meneja wa Chelsea Antonio Conte atatoa ombi jipya kwa klabu la kununua wachezaji wapya zaidi wiki ijayo baada ya kusema ana wasiwasi wa kufukuzwa kazi. Tayari Chelsea wametumia pauni milioni 130 msimu huu. (Sunday Telegraph)

Newcastle wanataka kumsajili Lucas Perez, 28, wa Arsenal na kumfanya kuwa mshambuliaji mkuu wa klabu hiyo, licha ya mchezaji huyo kutaka kurejea katika klabu yake ya zamani Deportivo La Coruna. (Sun on Sunday)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Tafadhali share tetesi hizi na wapenda soka wote. Nakutakia Jumapili njema.

Wednesday, July 26, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATANO 26.07.2017
Mancheter City wanajaribu kuwapiku Real Madrid katika kumsajili Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco. (Daily Mirror)

Manchester City wapo tayari kutoa pauni milioni 160 kumsajili Kylian Mbappe katika harakati za Pep Guardiola kujenga kikosi chake. (ESPN)

Kylian Mbappe ambaye alipachika mabao 15 katika mechi 29 za Ligue 1 msimu uliopita atakataa kwenda Manchester City akitaka kujiunga na Real Madrid. (Daily Star)

Manchester City hawajapanda dau lolote kumtaka Kylian Mbappe, na wala hawana mpango huo, ingawa Pep Guardiola amesema Real Madrid hawana ‘msuli’ mkubwa wa kifedha kama wa City. (Sky Sports)

Real Madrid wamefikia makubaliano na Monaco ya kumsajili Kylian Mbappe kwa euro milioni 180. (Marca)

Kiungo mshambuliaji wa Liverpool Philippe Coutinho anakaribia ’sana’ kujiunga na Barcelona (Mundo Deportivo)

Barcelona wametuma maafisa wake hapa England kujaribu kumsajili Philippe Coutinho, 25, licha ya Liverpool kukataa dau la pauni milioni 72. (Sports)

Liverpool wanasisitiza kuwa Philippe Coutinho hauzwi, lakini Barcelona wapo tayari kupanda dau la pauni milioni 80. (Daily Star)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema timu yake haiogopi ‘kumwaga fedha’ msimu huu huku wakiendelea kumsaka beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26. (Daily Mirror)

Liverpool wanatarajiwa kukamilisha usajili wa Virgil van Dijk kutoka Southampton ifikapo mwisho wa dirisha la usajili. (Sky Sports)

Arsenal hatimaye wanakaribia kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar, 21, kwa pauni milioni 45. (Sun)

Arsenal wanafikiria kumsajili kiungo wa Nice, Jean Michael Seri. (L’Equipe)

Arsenal wanakabiliwa na kupata hasara kwa mshambuliaji wake Lucas Perez, baada ya Deportivo La Coruna kutoa pauni milioni 9 kutaka kumsajili mchezaji huyo, 28. (Evening Standard)

Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25, anataka kubakia London iwapo ataondoka Emirates, huku West Ham ikionekana ni kimbilio lake. (Independent)

Stoke City wanataka kununua wachezaji kadhaa katika wiki chache zijazo, lakini hawana mpango wa kumtaka winga wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Stoke Sentinel)

Kiungo wa Bayern Munich Renato Sanches, 19, amesema anataka kuondoka Ujerumani huku AC Milan na Manchester United wakimnyatia mchezaji huyo mwenye thamani ya pauni milioni 43. (Independent)

Tottenham wanafikiria kumsajili beki wa Hoffenheim Jeremy Toljan, 22, baada ya mazungumzo ya kumsajili beki Ricardo Pereira, 23, wa Porto kukwama. (Daily Mail)

Everton wamepanda dau la pili la pauni milioni 45 kutaka kumsajili kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson. (The Telegraph)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.

Tuesday, July 25, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 25.07.2017
Meneja wa Chelsea Antonio Conte atakabidhiwa pauni milioni 150 zaidi za usajili huku akitaka kumchukua Virgil van Dijk, 26, kutoka Southampton na beki wa kushoto wa Juventus, Alex Sandro, 26. (Daily Mirror)

Kitita cha usajili cha Chelsea huenda kikafikia cha Manchester City cha pauni milioni 218. (Times)

Chelsea huenda wakatumia fedha zaidi wakati Antonio Conte akitaka kumsajili Antonio Candreva, 30, kutoka Inter Milan na pia mshambuliaji wa Swansea Fernando Llorente, 32 na pia kiungo wa Everton Tom Davies, 19. (Sun)

Chelsea vilevile wanataka kuwasajili Cedric Soares na Ryan Bertrand kutoka Southampton baada ya kumkosa Danilo na Benjamin Mendy. (Daily Star)

Chelsea wapo tayari kulipa euro milioni 40 za kutengua kifungu cha usajili ili kumchukua Sergi Roberto kutoka Barcelona. (Sport)

Mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28, yuko tayari kupunguziwa mshahara ili aweze kujiunga na Manchester City. Sanchez anapenda kwenda City kuliko Bayern Munich, PSG au Juventus. (Independent)

Arsenal na Liverpool huenda wakaamua kumsajili Karim Benzima, 29, iwapo Real Madrid wataamua kumuuza ili kumchukua Kylian Mbappe. Hata hivyo Real huenda wakamtumia Benzima pia kama chambo kwa Monaco ili kupunguza bei ya Mbappe. (Don Balon)

Liverpool wanamfuatilia kiungo wa kimataifa wa Poland, Sebastian Szymanski, 18, ambaye anachezea Legia Warsaw. (Polska Times)

Liverpool wamewaambia Crystal Palace watoe pauni milioni 30 kumchukua beki Mamadou Sakho, 27, na kuwa hawatokubali kumtoa kwa mkopo tena. (Daily Mirror)

Liverpool wametoa dau la pauni milioni 74 kumtaka kiungo wa RB Leipzig, Naby Keita, 22, baada dau mbili za awali kukataliwa. (Daily Star)

Emre Can amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na Juventus na anasubiri dau rasmi la pauni milioni 30.4 kutolewa ili kufanikisha uhamisho wake. (TMW)

Manchester City wamedhamiria kufunga dirisha la usajili kwa kumwaga fedha kwa kumsajili Alexis Sanchez, 28, au Kylian Mbappe, 18. Pep Guardiola hatoridhika mpaka ampate Sanchez anayedhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 50 au Mbappe ambaye ada yake inaweza kufika pauni milioni 100. (Daily Mail)

Roma wametoa pauni milioni 30 pamoja na marupurupu mengine kumtaka Riyad Mahrez, 26, lakini Leicester wanataka pauni milioni 50. (Daily Mail)

Riyad Mahrez, 26, Huenda akajikuta amebakia Leicester msimu ujao iwapo timu zinazomtaka ikiwemo Arsenal zitashindwa kutoa pauni milioni 50 kumsajili. (The Sun)

Everton wana uhakika wa kukamilisha usajili wa kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, kwa pauni milioni 45, ifikapo siku ya Alhamisi. (Daily Mail)

Manchester United huenda wakamsajili kiungo wa Bayern Munich Renato Sanchez, 19, kwa mujibu wa meneja Carlo Ancelotti, lakini Arturo Vidal, 30, haondoki kwa mabingwa hao wa Bundesliga. (Independent)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho atakataa dau lolote la kumtaka Ashley Young, 32, ambaye Stoke City wamekuwa wakimuulizia. (The Sun)

Galatasaray wanazungumza na Arsenal kuhusu kumsajili kiungo kutoka Misri Mohamed Elneny, 25. (Fotospor)

Paris Saint-Germain wamewapa Barcelona kiungo Marco Verratti pamoja na pauni milioni 90 juu, ili kumsajili Neymar. (Diario Gol)

Kiungo wa Chelsea Mason Hunt, 18, amesaini mkataba mpya wa miaka minne kabla ya kwenda Vitese kwa mkopo. (London Evening Standard)

Marseille wanazungumza na Celtic kutaka kumsajili mshambuliaji Moussa Dembele, 21, kwa pauni milioni 20. (Daily Express)

Borussia Dortmund wanataka kumsajili winga wa Manchester City Jadon Sancho, 17. (ESPN)

Winga wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele anataka kwenda Real Madrid baada ya kukata tamaa ya kusubiri dau kutoka kwa Barcelona. (Don Balon)

Mshambuliaji wa Arsenal Lucas Perez, 28, anataka kuondoka Emirates baada ya kuhisi “kusalitiwa” kufuatia namba yake ya jezi, 9, kupewa Alexandre Lacazette. (La Voz de Galicia)

Tottenham wamemkosa beki Juan Foyth, 19, ambaye anakaribia kujiunga na Paris Saint-Germain. (Squawka)

Swansea wamekubaliana na Manchester City kuhusu usajili wa Wilfried Bony, lakini wana wasiwasi na madai ya mshahara wa pauni 130,000 kwa wiki. Swansea wanahitaji mshambuliaji kutokana na uwezekano wa Fernando Llorente kuondoka kwenda Chelsea. (Wales Online)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.

Sunday, July 23, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 23.07.2017
Barcelona wapo tayari kutoa pauni milioni 80 kumtaka Philippe Coutinho, 25, kutoka Liverpool. (Sunday Mirror)

Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi, 30, ameiambia klabu yake kumsajili mshambuliaji wa Juventus Paulo Dybala, 23. (Don Balon)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema Coutinho “ametulia” Liverpool baada ya klabu hiyo kuzungumza naye kufuatia hatua ya Barcelona kumtaka. (ESPN FC)

Liverpool hatimaye wamefikia makubaliano na RB Leipzig ya pauni milioni 75 ili kumsajili Naby Keita. (Winner Sports)

Meneja wa Arsenal amekanusha taarifa kuwa Alexis Sanchez, 28, anakaribia kuhamia Paris Saint-Germain kwa pauni milioni 70. (Standard)

Alexis Sanchez anataka mshahara wa pauni 500,000 kwa wiki kutoka Paris Saint-Germain, huku akikaribia kuhamia Paris. (The Mirror)

Liverpool na Arsenal wameonesha dalili za kutaka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Lucas Vasquez. (Diario Madridista)

Chelsea wanapanga kuzungumza na Arsenal kuhusiana na Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Sky Sports)

Chelsea wanamfuatilia winga wa Montreal Impact Ballou Jean-Yves Talba, baada ya Didier Drogba kuwaambia kuhusu mchezaji huyo. (Sun)

Manchester United wana uhakika wa kumsajili kiungo wa Chelsea Nemanja Matic, 28, baada ya kumkosa Eric Dier, 23, wa Tottenham. (Guardian)

Mipango ya Manchester United kutaka kumsajili kiungo wa PSG, Marco Verratti, 24, kwa pauni milioni 60 imesitishwa kwa muda baada ya PSG kusema inamtaka Anthony Martial, 21. (Sunday Mirror)

Jose Mourinho amesema “ana uhakika” David de Gea atabakia Manchester United msimu huu, baada ya Real Madrid kushindwa kutumia nafasi ya kumsajili kipa huyo. (Sky Transfer Centre)

Manchester United sasa wamemgeukia kiungo wa Bayern Munich, Arturo Vidal, wakati wakitafuta kiungo mpya. (Daily Star)

Beki wa Manchester United Matteo Darmian, 27, amesema haendi popote licha ya taarifa kumhusisha na kurejea Italy. (Press Association)

Real Madrid wametengeneza orodha ya washambuliaji inayowataka, ikiwa watamkosa Kylian Mbappe. Miongoni mwao ni Marcus Rashford wa Manchester United, Pierre Emerick-Aubameyang wa Borussia Dortmund na Timo Werner wa RB Leipzig. (Diario Gol)

Real Madrid watamsajili mshambuliaji wa Ajax Kasper Dolberg pamoja na Domenico Berardi wa Sassuolo, iwapo watamkosa Kylian Mbappe. (Marca)

Real Madrid wamewaambia Monaco watawapa Karim Benzima kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Kylian Mbappe. (The Sun)

Chelsea wamemuulizia winga wa Inter Milan Antonio Candreva, ili kuogeza ushindani Stamford Bridge. (the Sun)

Kiungo wa Manchester City Kevin de Bruyne, 26, amesema ana matumaini klabu yake itanunua mabeki wengine kadhaa msimu huu. (Manchester Evening News)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na Jumapili njema.

Friday, July 21, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 21.07.2017
Dau la Manchester City la pauni milioni 44.5 la kumtaka beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 23, limekataliwa. Monaco wanataka pauni milioni 54. (Daily Mail)

Manchester City wapo tayari kumfanya Benjamin Mendy, 23, kuwa beki aghali zaidi duniani kwa kumsajili kutoka Monaco. (L’Equipe)

Manchester City watakamilisha usajili wa Danilo, 26, kutoka Real Madrid siku ya Ijumaa. (Marca)

Beki wa Manchester City Aleksander Kolarov anakaribia kujiunga na Roma, kwa mujibu wa meneja wake Pep Guardiola. (Sky)

Barcelona wamewasilisha dau la pauni milioni 72 kumtaka kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, lakini Liverpool wanatarajiwa kutupilia mbali dau hilo. (Daily Mail)

Liverpool wamesema Barcelona wanapoteza muda wao kutaka kumsajili Philippe Coutinho, 25. (Liverpool Echo)

Juventus wanataka kuimarisha kiungo chao kwa kumsajili Emre Can kutoka Liverpool. (Gianluca Dimarzio)

Arsenal wana uhakika kuwa kiungo wao Mesut Ozil, 28, atasaini mkataba mpya kubakia Emirates. (Sun)

Manchester United sasa wameelekeza nguvu zao kumtaka beki wa kulia wa Paris Saint-Germain, Serge Aurier, 24, kutokana na kusuasua kwa mipango ya kumsajili Fabinho, 23, kutoka Monaco. (Independent)

Meneja wa PSG Unai Emery amethibitisha kuwa Serge Aurier anataka kuondoka Paris msimu huu. (L’Equipe)

Manchester United wanataka kuwazidi kete AC Milan katika kumsajili Renato Sanches kutoka Bayern Munich. (The Guardian)

Manchester United bado hawajafikia dau wanalotaka Inter Milan katika kumsajili Ivan Perisic, 28. (Daily Mirror)

Jose Mourinho ameitaka klabu yake ya Manchester United kumsaidia kusajili mchezaji mmoja tu zaidi “haraka iwezekanavyo”. (Sky Sports)

Wolfsburg wameulizia uwezekano wa kumsajili mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial. (Kicker)

Diego Costa huenda akacheza kwa mkopo AC Milan, wakati akisubiri kuhamia Atletico Madrid. (Don Balon)

Chelsea wapo tayari kumuuza Diego Costa kwenda Atletico Madrid kwa pauni milioni 44, na sio pauni milioni 25 zilizotolewa na Atletico. (Independent)

Alexis Sanchez, 28, amefikia makubaliano na Paris Saint-Germain, na klabu hiyo ya Ufaransa itapanda dau la pauni milioni 45. Kinachosubiriwa ni kauli ya Arsene Wenger. (Sun)

Kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25, yuko tayari kwenda West Ham, iwapo klabu hiyo itafikia makubaliano kuhusu ada ya uhamisho. (Daily Star)

Arsenal wamekataa dau la pauni milioni 16, la kumsajili beki wake Callum Chambers. Arsenal wanataka pauni milioni 20. (Daily Telegraph)

Tottenham wametaka kufahamishwa msimamo wa Riyad Mahrez, lakini Leicester watalazimika kupunguza bei ya pauni milioni 50, kama watamuuza kwenda White Hart Lane. (Standard)

Wachezaji wa Leicester City wapo tayari ‘kumhamasisha kwa lazima’ Riyad Mahrez ikiwa hatajituma kwa asilimia 100, amesema kiungo Andy King. (Leicester Mercury)

Meneja wa Leicester City Craig Shakespeare amethibitisha kuwa wamekataa dau kutoka Roma la kumtaka Riyad Mahrez. (Sky Transfer Centre)

Arsenal na Tottenham zinamnyatia winga kinda wa Manchester City Jadon Sancho, 17. (Independent)

Mshambuliaji wa Stoke City, Marco Arnautovic, 28, atakuwa mchezaji anayelipwa zaidi West Ham baada ya kukamilisha vipimo vyake vya afya siku ya Ijumaa. (Daily Express)

Torino wanataka AC Milan itoe euro milioni 50 pamoja na M’Baye Niang, Gabriel Paletta na Manuel Locatelli, kama wanamtaka Andrea Belotti. (La Stampa)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumaa Kareem.

Thursday, July 20, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 20.07.2017
Paris Saint-Germain wanajiandaa kuzungumza na Barcelona kuhusu uhamisho wa pauni milioni 196 wa Neymar, 25. (Guardian)

PSG wapo tayari kumpa Neymar pauni milioni 45, za kukubali tu kujiunga nao, na mshahara wa pauni 596,000 kwa wiki (baada ya makato ya kodi) na mkataba wa miaka mitano. (Daily Mail)

Barcelona wanapanga kuzungumza na Monaco kuhusu kumsajili Kylian Mbappe, 18. Barca wanatarajia kupata fedha za kutosha kumsajili Mbappe baada ya kumuuza Neymar, 25. (Daily Mail)

Chelsea wanataka pauni milioni 44 kutoka kwa Atletico Madrid kwa ajili ya Diego Costa, 28, baada ya kukamilisha usajili wa Alvaro Morata, 24, kutoka Real Madrid. (Independent)

Rais wa Atletico Madrid Enrique Cerezo amesema hakuna uhakika thabiti iwapo Diego Costa atakwenda Atletico Madrid. (Mirror)

Chelsea, Tottenham na Manchester United huenda zikaingia katika mapambano ya kumgombania kiungo wa Everton Ross Barkley, 23. (The Times)

Liverpool wapo tayari kutoa pauni milioni 70 kumsajili kiungo wa RB Leipzig Naby Keita, 22, baada ya dau la pauni milioni 66 kukataliwa. (Mirror)

West Ham wanakaribia kukamilisha usajili wa mshambuliaji wa zamani wa Manchester United Javier ‘Chicharito’ Hernandez, 29, kutoka Bayer Leverkusen. (Sky Sports)

Arsenal wamewaambia West Ham kuwa watalazimika kutoa pauni milioni 20 ikiwa wanamtaka kiungo Jack Wilshere, 25. (Daily Star)

Paris Saint-Germain wamemtuma mkurugenzi wao wa michezo kwenda London kujaribu kumshawishi Alexis Sanchez, 28, ambaye pia anasakwa na Manchester City. (Sun)

Everton wamepata matumaini zaidi ya kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud, 30. (The Telegraph)

Kiungo wa Arsenal Mohamed Elneny amekataa kuhamia Leicester City waliokuwa tayari kutoa pauni milioni 10 kumsajili. (The Sun)

Manchester City wanakaribia kumsajili beki wa Real Madrid Danilo, 26, kwa pauni milioni 26.5. (Guardian)

Manchester city wanakaribia kukamilisha usajili wa beki Benjamin Mendy, 23, kutoka Monaco. (Times)

Manchester United wanahusishwa na kutaka kumsajili kiungo wa Paris Saint-Germain, Marco Verratti, 24, baada ya mchezaji huyo kumfanya Mino Raiola kuwa wakala wake mpya. (Sun)

Manchester United na Chelsea zilitazama uwezekano wa kumsajili Neymar, lakini timu hizo mbili zilikatishwa tamaa na bei ya pauni milioni 196 ya mchezaji huyo, 25, kutoka Brazil. (Independent)

Inter Milan wamewaambia Manchester United lazima wamjumuishe Anthony Martial, 21, katika mkataba wowote utakaohusu uhamisho wa Ivan Perisic, 28. (Independent)

AC Milan wamesema kiungo mshambuliaji wao Suso, 23, anayenyatiwa na Tottenham, hauzwi. (Tuttomercato)

PSG watamuuza kiungo Blaise Matuidi, 30, iwapo dau zuri litatolewa. (L’Equipe)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na siku njema.

Saturday, July 15, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 15.07.2017
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekuwa akimtumia ujumbe mfupi wa maandishi Alexis Sanchez, 28, kujaribu kumshawishi asiondoke Emirates. (Sun)

Mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe ameonesha dalili za kuondoka katika klabu yake hiyo huku Arsenal wakiendelea kumnyatia. (Marca)

Chelsea wana uhakika wa kuwapiku Liverpool katika kumsajili Pierre Emerick-Aubameyang, 28, kutoka Borussia Dortmund, ambao sasa wameanza mazungumzo ya kumtaka Olivier Giroud wa Arsenal. (Daily Mirror)

Nemanja Matic, 28, huenda akajiunga na Juventus baada ya Chelsea kumruhusu kutojiunga na kikosi kinachokwenda China na Singapore kwa ajili ya mechi za kujiandaa na msimu mpya. Diego Costa pia ameachwa. (Guardian)

Arsenal wameonesha dalili za kumtaka Nemanja Matic, na wapo tayari kubadilishana na Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Calcio Mercato)

Kasper Schmeichel, 30, amepata matumaini ya kujiunga na Manchester United baada ya taarifa kuwa Real Madrid wamepanda dau la kumtaka David de Gea, 26. (Daily Mirror)

Manchester United wana uhakika Real Madrid hawataiweza bei ya David de Gea. (ESPN)

Iwapo David de Gea atakwenda Real Madrid, meneja wa Manchester United atataka mchezaji mmoja kutoka Real na huenda akamtaka beki Rafael Varane. (Don Balon)

Kipa namba tatu wa Manchester United, Joel Pereira, 21, ana nafasi ya kuwa namba moja iwapo De Gea ataondoka. (Independent)

Inter Milan huenda wakamuulizia mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial wamchukue kwa mkopo kama sehemu ya mkataba wa United kumsajili Ivan Perisic, 28. (Daily Telegraph)

Tottenham watachuana na Juventus katika kumsajili beki wa Porto Ricardo Pereira, na watatazamiwa kulipa pauni milioni 22, kumchukua mchezaji huyo kuziba pengo la Kyle Walker. (Evening Standard)

Joe Hart anakaribia kukamilisha usajili wake wa pauni milioni 10 kutoka Manchester City kwenda West Ham. (Manchester Evening News)

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho hatoishutumu bodi ya klabu kwa kushindwa kumsajili Alvaro Morata. (Daily Express)

Liverpool huenda wakapanda dau la pauni milioni 65 kutaka kumsajili kiungo wa RB Leipzig Naby Keita, 22. (Liverpool Echo)

Roma wanajiandaa kupanda dau la pauni milioni 30 kumtaka winga wa Leicester Riyad Mahrez, 26. (Goal)

Meneja wa Birmingham Harry Redknapp anataka kumsajili beki wa zamani wa Arsenal na Chelsea, Ashley Cole, 36, kutoka LA Galaxy. (Sun)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumamosi njema.

Friday, July 14, 2017

Tetesi

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 14.07.2017
Liverpool na Chelsea wanataka kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick-Aubameyang, 28, ambaye thamani yake ni pauni milioni 65. (Sun)

Dortmund wamemuambia Aubameyang kuamua anataka kwenda wapi kabla klabu hiyo haijaingia kambini nchini Uswisi Julai 24. (Sun)

Kipa wa Manchester United David de Gea, 26, anataka kujiunga na Real Madrid msimu huu na amemuambia wakala wake Jorge Mendes kufanikisha uhamisho wake. (Don Balon)

Manchester City wapo tayari kutoa pauni milioni 50 kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22. (Daily Mirror)

Chelsea watakamilisha usajili wa kiungo Tiemoue Bakayoko, 22, kutoka Monaco kwa pauni milioni 39.7 katika saa 24 zijazo, ingawa mchezaji huyo atakosa mechi kadhaa za mwanzo kutokana na kuwa majeruhi. (Daily Express)

RB Lepzig wamekataa dau la pauni milioni 57 kutoka Liverpool la kumtaka kiungo Naby Keita, 22. (Bild)

Kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, atakataa kwenda Leicester kwa sababu anataka kujiunga na Everton. (Leicester Mercury)

West Ham wanakaribia kukamilisha usajili wa mkopo wa kipa wa Manchester City Joe Hart, 30. (Independent)

Newcastle watapewa nafasi ya kumsajili kipa wa West Ham Darren Randolp, ikiwa Joe Hart atakwenda West Ham. (Newcastle Chronicle)

Barcelona wameacha kumfuatilia beki wa Arsenal Hector Bellerin, 22, baada ya klabu hiyo ya Uhispania kufikia makubaliano ya kumsajili Nelson Semedo, 23 kutoka Benfica. (London Evening Standard)

Roma wametoa dau la pauni milioni 29 kumtaka Riyad Mahrez, 26, lakini Leicester wanataka pauni milioni 50. (London Evening Standard)

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anataka uhamisho wa Kyle Walker, 27, kwenda Man City uharakishwe ili wapate fedha za kusajili wachezaji wengine. (Daily Mail)

Tottenham wanatarajia kuziba pengo la Kyle Walker kwa kumsajili beki wa Porto Rocardo Pereira, 23, kwa pauni milioni 22. (Times)

Tottenham wanakaribia kukamilisha usajili wa beki Juan Foyth, 19, kutoka Estudiantes, ambaye atakuwa usajili wa kwanza wa Spurs msimu huu. (ESPN)

Tianjin Quanjian wamempa mkataba wa pauni milioni 26 kwa mwaka, mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24. (Onda Cero)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Ijumaa Kareem.

Thursday, July 13, 2017

Tetesi

TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 13.07.2017
Chelsea wameambiwa wanaweza kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick-Aubameyang, 28, kwa pauni milioni 60 baada ya Tianjin Quanjian ya China kusema haitaki tena kumsajili mchezaji huyo. (Daily Mail)

Borussia Dortmund huenda wakaamua kumfuatilia mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud, 30, ambaye pia anasakwa na Everton, West Ham, Marseille na AC Milan. (Daily Mirror)

Mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, 26, amempigia simu meneja wa Real Madrid Zinedine Zidane na kumuambia hana mpango wa kuondoka Chelsea msimu huu. (Diario Gol)

Chelsea wamefikia makubaliano na Monaco ya kumsajili kiungo Tiemoue Bakayoko, 22, kwa pauni milioni 40 kwa mkataba wa miaka mitano. (RMC)

Meneja wa Chelsea anajiandaa kumuuza kiungo Nemanja Matic, 28, kwa pauni milioni 40. Matic amekuwa akifanya mazoezi peke yake na anataka kuungana na Jose Mourinho Old Trafford. (Daily Telegraph)

Barcelona wanataka kumsajili beki wa Chelsea Cesar Azpilicueta baada ya kushindwa kumpata Hector Bellerin wa Arsenal. (Marca)

Chelsea watawazidi kete Juventus katika kumsajili beki wa kulia wa Real Madrid Danilo, 25, kwa pauni milioni 28. (Daily Mirror)

Mchezaji wa zamani wa Liverpool Danny Murphy amesema klabu hiyo inakaribia kukamilisha usajili wa Virgil van Dijk, 26, kutoka Southampton. (Sports360)

Arsenal wana uhakika dau la pauni milioni 45 litatosha kumsajili winga wa Monaco Thomas Lemar, 21. (Daily Mail)

Arsenal wanataka kumsajili kinda wa West Ham Domingos Quina, 17. (Sky Sports)

Roma wanataka kumsajili winga wa Leicester City Riyad Mahrez, 26. (Sky Italia)

Tottenham wamesema hawatoburuzwa na Manchester United na Manchester City kuhusu usajili wa Eric Dier na Kyle Walker, huku wakikaribia kumsajili beki Juan Foyth, 19, kutoka Estudiantes kwa pauni milioni 9. (Daily Telegraph)

Manchester United wana matumaini ya kukamilisha usajili wa winga wa Inter Milan Ivan Persic, 28, wiki ijayo. (Daily Star)

Manchester United sasa wataelekeza nguvu zao kumsajili kiungo wa Roma Radja Nainggolan, 29, kwa kutoa pauni milioni 40 baada ya Tottenham kukataa dau lolote kuhusu Eric Dier. (Daily Mail)

Leicester City huenda wakaondoa wachezaji sita waliosajiliwa msimu uliopita akiwemo Islam Slimani, 29, na Ahmed Musa, 24, pamoja na kiungo Nampalys Mendy, 25. (Daily Telegraph)

Middlesbrough wamewazidi kete Burnley na Watford katika kumsajili Britt Assombalonga, 24, kwa pauni milioni 14 kutoka Nottingham Forest. (Sun)

West Ham wanafikiria kupanda dau la tatu kumtaka Marco Arnautovic, 28, baada ya dau la pauni milioni 20 kukataliwa na Stoke City. (London Evening Standard)

Watford na Swansea zinamtaka kiungo wa Chelsea Nathaniel Chalobah, 22. (Sun)

Real Madrid wamekata tamaa ya kumpata kipa wa Manchester United David de Gea, 26, msimu huu. (Daily Star)

Manchester City wanakaribia kumsajili kiungo kutoka Brazil Douglas Luiz, 19, anayechezea Vasco da Gama. (ESPN)

Manchester City wanataka kupanda dau la pauni milioni 25 kumtaka beki wa Southampton Ryan Bertrand, 27, baada ya kumkosa Dani Alves aliyesaini PSG. (Daily Mail)

Stoke City watawazidi kete West Brom katika kumsajili beki wa Chelsea Kurt Zouma, 22 kwa mkopo. (Sun)
Fenerbahce ya Uturuki inataka kumsajili mshambuliaji wa Chelsea Michy Batshuayi, 23. (Fanatik)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na siku njema.

Tuesday, July 11, 2017

Usajili

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE 11.07.2017
Chelsea wanakaribia kukamilisha usajili wa kiungo wa Monaco Tiemoue Bakayoko, 22, na huenda akasaini mkataba wake kabla ya Jumatatu na kusafiri na timu kwenda Singapore na China (Sky Sports).

Manchester United wanataka kupanda dau zaidi ya la Chelsea na kumsajili Tiemoue Bakayoko kwa pauni milioni 40 (Daily Mail).

Meneja wa Manchester United Jose Mourinho pia anataka klabu hiyo kutoa dau la pauni milioni 60 ili kutaka kumsajili kiungo wa Tottenham Eric Dier 23 (Mirror).

Manchester United hawatomuongeza mkataba Zlatan Ibrahimovic, 35, licha ya kumruhusu kuendelea kutumia uwanja wa mazoezi wa klabu hiyo wa Carrington wakati akiuguza jeraha lake la goti (Star).

Manchester United bado hawajaweza kutoa kiasi wanachotaka Inter Milan ili kumsajili winga Ivan Perisic, 28, lakini wanatazamia kukamilisha mkataba wa pauni kati ya milioni 45 hadi 50 (Independent).

Arsenal wana uhakika wa kutomuuza kiungo Alex Oxlade-Chamberlain, 23 ambaye amebakiza miezi 12 tu kwenye mkataba wake wa sasa (Daily Mail).

Meneja wa Arsenal Arsene Wenger pia amedhamiria kutomuuza Alexis Sanchez, 28, ambaye hajasaini mkataba mpya na inadhaniwa anataka kwenda Manchester City (Independent).

Arsene Wenger hataki kumuuza Olivier Giroud, 30, mpaka suala la Alexis Sanchez na Thomas Lemar litakapotatuliwa (Daily Telegraph).

Arsenal watapambana na Liverpool katika kutaka kumsajili beki wa Southampton Virgil van Dijk, 26 (Sun).

Chelsema wameweka kipaumbele katika kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24, huku kukiwa hakuna uhakika na hatma ya Diego Costa, 28 (Guardian).

Diego Costa yuko tayari kuichezea Chelsea na kufikia muafaka na meneja wake Antonio Conte (Star).

Roma wanataka kumchukua kwa mkopo mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial, 21, lakini Old Trafford huenda wakapinga hatua hiyo (Mirror).

Manchester City wapo tayari kutoa pauni milioni 27 kumsajili beki wa kati wa Real Sociedad Inigo Martinez, 26 (Marca).

Meneja wa Leicester amekuwa na mazungumzo na winga Demarai Gray, 21, na anataka mchezaji huyo asiondoke huku Liverpool, Tottenham na Everton zikimtaka (Sky Sports).

Leicester City wamekubaliana kimsingi na Manchester City kuhusu kumsajili mshambuliaji Kelechi Iheanacho, 20 (Sky Sports).

James Rodriguez, 26, anataka hatma yake ifahamike mara moja, huku Real Madrid wakitaka pauni milioni 62. Manchester United na timu kadhaa Ulaya zimeambiwa zinaweza kupanda dau (Mail).

Tottenham watakuwa na mazungumzo na Estudiantes wiki hii kuhusiana na usajili wa beki Juan Foyth, 19 (London Evening Standard).

Deportivo La Coruna hawana uhakika kama wataweza kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Lucas Perez, 28, msimu huu (FourFourTwo).

Burnley wanafikiria kumsajili kiungo wa Swansea Jack Cork, 28, lakini wamesema hawamtaki kiungo wa Stoke Glenn Whelan, 33 (Lancashire Telegraph).

Newcastle wanafikiria kumchukua kipa wa Paris Saint-Germain Alphonce Areola, 24 (France Football).

Newcastle watamkosa winga wa Manchester City Jesus Navas, 31, ambaye anakaribia kurejea Sevilla (Marca).

Meneja wa Newcastle Rafael Benitez ametaka klabu yake kuongeza dau katika kumsajili winga wa Norwich Jacob Murphy (Daily Telegraph).

Paris Saint-Germain wanasubiri kuona kama wamefanikiwa kumshawishi Dani Alves, 34, asiende Manchester City (Daily Mail).

Brighton wanataka kumsajili kiungo wa Chelsea Izzy Brown, 20 (Brighton & Hove Independent).

Chelsea wanajiandaa kutoa pauni milioni 70 kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24 (AS).

Inter Milan watapambana na Manchester United kutaka kumsajili kiungo wa Chelsea Nemanja Matic, 28 (Corriere dello Sport).

Tottenham nao wanamtaka mshambuliaji wa Manchester City Kelechi Iheanacho, 20 (The Sun).

Newcastle wamemuulizia winga wa Middlesbrough Adama Troure, 21 (Chronicle).

Everton wanafikiria kumchukua mshambuliaji wa Crystal Palace Christian Benteke kuziba nafasi ya Romelu Lukaku. Everton pia wanamtaka Olivier Giroud au Edin Dzeko (Daily Mail).

Manchester United walikataa nafasi ya kumsajili Alexandre Lacazette na badala yake wakaamua kumfuatilia Romelu Lukaku (The Guardian).

Dani Alves bado hajaamua aende wapi huku Manchester City, Chelsea na Tottenham zikimtaka (Globo Esporte)

Atletico Madrid wamekubaliana mkataba wa euro milioni 45 na Monaco wa kumsajili Fabinho ambaye amehusishwa na Manchester United, PSG na Manchester City, lakini huenda akajiunga na Atletico baada ya adhabu yao kumalizika (AS).

Liverpool bado wanavutana na mshambuliaji wa Atletico Madrid Angel Correa ambaye ada yake ya uhamisho ya pauni milioni 25 imekubaliwa lakini mchezaji huyu anataka mshahara mkubwa kuliko Liverpool wanaotaka kutoa (Foot Mercato).

Chelsea wanataka kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick-Aubameyang, 28, baada ya kumkosa Romelu Lukaku na wapo tayari kulipa euro milioni 70 (Marca).

Marseille wanamtaka mshambuliaji wa Manchester City Wilfried Bony (The Sun).

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Tafadhali share tetesi hizi na wapenda soka wote. Uwe na siku njema.

Monday, July 10, 2017

Usajili

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU 10.07.2017
Everton wametoa dau jipya la pauni milioni 32 kumtaka kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27. Wakifanikiwa watakuwa wametuia zaidi ya pauni milioni 100 za usajili msimu huu (Daily Mail).

Baada ya kumsajili Romelu Lukaku, 24, kutoka Everton, Manchester United huenda wakamsajili kiungo wa Monaco Tiemoue Bakayoko, 22, baada ya kukubaliana mkataba wa pauni milioni 35. Chelsea wanamtaka pia Bakayoko (Daily Star).

Arsenal wapo tayari kupanda dau la tatu la zaidi ya pauni milioni 45 kumtaka winga wa Monaco, Thomas Lemar, baada ya dau la pauni milioni 30 na 40 kukataliwa (Daily Mirror).

Mshambuliaji wa Arsenal Theo Walcott, 28, amedhamiria kupigania nafasi yake Emirates, licha ya kuhusishwa na kuhamia West Ham kwa pauni milioni 20 (Daily Star)

Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger anataka kuimarisha eneo la kiungo kwa kumsajili Marcelo Brozovic kutoka Inter Milan (ESPN).

Kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny, 27,  ambaye amehusishwa na kuhamia Juventus, ameachwa kwenye kikosi kilichosafiri kwenda Australia kwa ajili ya mechi za kujiandaa na msimu mpya (Sun).

Chelsea wapo tayari kutoa euro milioni 80 kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid, Alvaro Morata baada ya kumkosa Romelu Lukaku (AS).

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anataka kumsajili beki wa Estudiantes, Juan Foyth, 19 kwa pauni milioni 10 (Daily Mirror).

Real Madrid wapo tayari kumuuza kiungo Mateo Kovacic, na Tottenham wamehusishwa na kumchukua mchezaji huyo wa kimataifa wa Croatia (Evening Standard).

Cristiano Ronaldo atabakia Real Madrid msimu wa 2017-18 na hivyo kufuta uvumi wa kuhamia Manchester United (AS).

Newcastle wanajaribu kukamilisha usajili wa kiungo wa Norwich Jacob Murphy, 22, kwa pauni milioni 8.5, huku Southampton na Crystal Palace wakimtaka pia mchezaji huyo (Daily Mirror).

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.

Saturday, July 8, 2017

Usajili

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI 08.07.2017
Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa, 28, yuko tayari kuwa na mazungumzo na Antonio Conte, na huenda akaichezea tena klabu hiyo msimu ujao. Costa alitumiwa ujumbe mfupi wa simu (SMS) na Conte kuambiwa kuwa hahitajiki tena Stamford Bridge (Sun).

Chelsea wanataka zaidi ya pauni milioni 60 kumuuza Diego Costa, na watamuuza hata ikiwa Romelu Lukaku ataamua kujiunga na Manchester United (Daily Mail).

Huku Romelu Lukaku akikaribia kujiunga na Manchester United, Chelsea sasa huenda wakaelekeza nguvu zao kumtaka Andrea Belotti, 23, kutoka Torino na watalazimika kulipa takriban pauni milioni 90 (Daily Mirror).

Mkataba wa Romelu Lukaku kutoka Everton kwenda Manchester United ni pauni milioni 75 za awali na ada hiyo itapanda hadi pauni milioni 90 (Sky)

Antonio Conte sasa anataka kumsajili mshambuliaji wa zamani wa Man Utd Javier “Chicharito” Hernandez kwa pauni milioni 13.5 baada ya dau lao la dakika za mwisho kutaka kumsajili Lukaku kushindikana (The Sun).

Wayne  Rooney anajiandaa kukata mshahara wake kwa nusu hadi pauni 150,000 kwa wiki kujiunga na Everton kutoka Manchester United (Daily Mail).
Wayne Rooney amekubali kusaini mkataba wa miaka miwili kwenda Everton kutoka Manchester United (Daily Star).

Manchester United wataelekeza nguvu zao kumtaka kiungo wa Tottenham Eric Dier, 23, kwa pauni milioni 50 mara watakapokamilisha mkataba wa Lukaku (Telegraph).

Manchester United wameongeza bidii katika mazungumzo ya kutaka kumsajili kiungo wa Real Madrid James Rodriguez (The Independent).

Manchester United watalazimika kusubiri hadi mwezi Januari kupanda dau kumtaka beki wa kulia wa Benfica Nelson Semedo (Correio da Manha).

Arsenal wanasubiri jibu kutoka Monaco kuhusu kupanda dau la pauni milioni 40 kumtaka winga Thomas Lemar, 21 (Football London).

Arsenal wanamtaka kipa wa Toulouse Alban Lafont, 18, ili kuwa mrithi wa Petr Cech, pia wanamfuatilia kipa Stephane Ruffier wa St Etienne (Le 10).

Meneja wa Leicester City Craig Shakespeare amemuambia winga Riyad Mahrez , 26 anayehusishwa na kuhamia Arsenal kuwa hatocheza ikiwa haoneshi kujituma (Daily Telegraph).

Arsenal hawatomuuza Alexis Sanchez, 28, au Alex Oxlade-Chamberlain, 23, kwa timu yoyote ya EPL, licha ya kuwa wachezaji hao wanakaribia mwisho wa mikataba yao (Daily Star).

Alexis Sanchez ameiambia Arsenal kuwa anataka kuondoka na kwenda Manchester City. Makubaliano yamefikiwa kati ya Sanchez na City kwa pauni milioni 46.5, lakini Arsenal wanasita kumuuza kwa timu hasimu ya EPL, lakini huenda akaondoka bure mwisho wa msimu ujao (El Mercurio).

Crystal Palace wanataka kupanda dau kumtaka kipa wa Barcelona Jasper Cillesen, 28, (AS).

Paris Saint-Germain wanaongoza mbio za kumsajili Gareth Bale kutoka Real Madrid (Don Balon).

West Ham wamepunguza kasi ya kutaka kumsajili kipa wa Man City Joe Hart na sasa wanatafuta mshambuliaji (Sun).

Liverpool wanasema timu kadhaa zimemuulizia beki wake Mamadou Sakho, na wana uhakika kuna timu itaweza kulipa pauni milioni 30 (Liverpool Echo).

Mshambuliaji wa Man City Wilfried Bony anavutia timu kadhaa za China na City wana imani watapata pauni milioni 14 kwa mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast (Independent).

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na siku njema.

Friday, July 7, 2017

Usajili

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 07.07.2017
Mustakbali wa meneja wa Chelsea, Antonio Conte uko mashakani baada ya meneja huyo kukasirishwa na shughuli nzima ya usajili katika klabu hiyo (Daily Mirror).

Hatua ya Manchester United kutaka kumsajili Romelu Lukaku, 24, haihusiani na mkataba ambao utamrejesha Wayne Rooney, 31, Everton (Liverpool Echo).

Chelsea bado wanatarajiwa kujaribu  kumsajili Romelu Lukaku, 24, licha ya taarifa kuwa mchezaji huyo amekubali kuhamia Manchester United kwa pauni milioni 75 kutoka Everton (Guardian).

Mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24, ameachwa “kwenye mataa” baada ya Manchester United kumsajili Romelu Lukaku. Morata alikuwa na uhakika kuwa anahamia Old Trafford (Independent).

Romelu Lukaku amekubali kusaini mkataba wa muda mrefu Manchester United na mshahara wa pauni 250,000 kwa wiki (Daily Star).

Chelsea huenda wakakabiliwa na tatizo la mshambuliaji baada ya Diego Costa kuanza kuaga wachezaji wenzake kufuatia kuambiwa na Antonio Conte kuwa hayuko kwenye mipango yake msimu ujao (Daily Telegraph).

Chelsea wanajiandaa kutoa dau “kubwa” kumtaka kiungo wa Real Madrid James Rodriguez (AS).

Chelsea sasa wameelekeza macho yao kwa mshambuliaji wa Swansea Fernando Llorente, 32, baada ya kushindwa kumpata kwa mkopo mwezi Januari (Evening Standard).

Barcelona wamekasirishwa na nahodha wao wa zamani Carles Puyol, baada ya mchezaji anayemwakilisha Eric Garcia, 16, kuamua kuhamia Manchester City (Independent).

Everton wanajiandaa kupanda dau jipya la pauni milioni 32 kumtaka kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27 (Daily Mail).

Kipa wa Stoke City Jack Butland, 24, amesema anaweza ‘kufikiria’ iwapo Manchester United watamtaka (Manchester Evening News).

Arsenal wanamtaka kiungo wa Eintracht Frankfurt Aymen Barkok, 19 (Spox).

Marseille wanaongoza katika mbio za kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud, 30, kwa kitita cha pauni milioni 24.7, baada ya Arsenal kufanikisha usajili wa Alexandre Lacazette (Daily Telegraph).

Arsenal hawataki kulipa kiasi ambacho Leicester wanakitaka ili kumsajili winga Riyad Mahrez, 26, ambaye anatarajiwa kuondoka Leicester msimu huu (Daily Star).

Barcelona wapo tayari kutoa pauni milioni 26 kumsajili beki wa Arsenal Hector Bellerin (Sport).

Arsenal wanamfuatilia kiungo wa Monaco Fabinho (France Football).

Winga wa zamani wa Newcastle Hatem Ben Arfa, 30, ameambiwa anaweza kuondoka Paris Saint-Germain (L’Equipe).

Paris Saint-Germain watamgeukia Philippe Coutinho iwapo watashindwa kumsajili Kylian Mbappe kutoka Monaco. PSG wapo tayari kutoa pauni milioni 70 kumchukua Coutinho (Le10sport).

Winga Demarai Gray, 21, anataka kuhakikishiwa namba Leicester huku Tottenham na Liverpool zikimnyatia (Daily Mirror).

Dau la pauni milioni 22 la Barcelona kumtaka kiungo wa zamani wa Tottenham, Paulinho, 28, limekataliwa na klabu yake ya Guangzhou Evergrande (Sky Sports).

Licha ya Guangzhou Evergrane kukataa, Barcelona watarejea na dau jingine kumtaka Paulinho (Cadena SER).

Stoke City wamekuwa na mazungumzo na Manchester City ya kumsajili kiungo Fabien Delph, 27 (Stoke Sentinel).

Real Madrid wamekuwa na mazungumzo ya siri na PSG kuhusu Marco Verratti,24 (Don Balon).

Real Madrid wamekuwa na mazungumzo mapya na Kylian Mbappe (Marca).

Real Madrid watakuwa tayari kumruhusu Gareth Bale kuondoka kwa pauni milioni 88 (Diario Gol).

Watford wanazungumza na Chelsea kuhusu kiungo Nathaniel Chalobah, 22, na wana uhakika mchezaji huyo anataka kurejea Vicarage Road (London Evening Standard).

Aston Villa wamemuulizia kipa wa Manchester City Joe Hart (Birmingham Mail).

AC Milan sasa wamemgeukia mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick-Aubameyang, 28, na pia wanamtaka Nikola Kalinic (Gianluca Di Marzio).

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na siku njema.