Tuesday, March 29, 2016

Mshukiwa wa brussels aachiwa huru

aachiwa huru Afisi ya kiongozi wa mashtaka nchini Ubelgiji imemuachilia huru mshukiwa mkuu wa mashambulio ya bomu yaliyotokea juma lililopita jijini Brussels. Kingozi wa mashtaka ya umma anasema hakuna ushahidi wa kuthibitisha kuwa mtu anayetambuliwa kama Faycal C ndiye mshukiwa mkuu aliyenaswa na kamera fiche (CCTV) katika eneo lililoathirika. Afisi hiyo inasema hadi kufikia sasa hizo zilikuwa ni madai tu dhidi ya bwana huyo. Faycal C alikamatwa baada ya mtu kuielezea polisi kuwa alimshuku kuwa ndiye aliyeonekana katika picha fiche CCTV katika uwanja wa ndege wa Zaventem muda mchache kabla ya mlipuko huo uliosababisha maafa makubwa. Kufuatia kauli hiyo polisi wamechapisha upya picha za mshukiwa aliyeonekana akiandamana na washambuliaji wa kujitolea mhanga akiwa amevalia kofia. Image Image Kufuatia kauli hiyo polisi wamechapisha upya picha za mshukiwa aliyeonekana akiandamana na washambuliaji Kauli hiyo ya afisi ya kiongozi wa mashtaka imetupilia mbali matumaini ya kumkamata mshukiwa halisi aliyekwepa kutoka eneo la tukio baada ya shambulizi lililoua zaidi ya watu 35. Ibaada ya makumbusho imeratibiwa kufanyika usiku kutwa katika kanisa kuu mjini Brussels.

Saturday, March 26, 2016

Wkb

****Worth Reading**** Great advice from the Richest person in China Mr. Jack Ma. Jack Ma says, "Please tell your children that the world is changing every day and no one is going to wait for you in the past. When lighter was invented, matches slowly disappeared. When calculator was created, abacus was to fade away. When digital camera was designed, the market of negative film no longer existed. When direct market selling/internet-based selling arises, traditional marketing declines. When smartphone with 4G (wireless internet access) was introduced to the world, you no longer need to turn on your computer at home. When WeChat and WhatsApp (mobile text/voice/video messaging) are developed, traditional text messaging is no longer as popular as before. Let's not to blame "Who took over Whose business." It's only because people are more adjustable and adaptable to new ideas and changes in the world. Someone asks Jack Ma, "What is your secret for success?" He says, "Really simple...I am doing (action) while you're only watching." Please remember that the world keeps changing every day. If you don't change, you'll be left behind. You reap what you sow with your time. If you spend time to drink, you may become an alcoholic. If you spend time to complain, you may become a blamer. If you spend time to beautify yourself, you may become a pretty girl/handsome guy. If you spend time to stay healthy, you may enjoy a healthy good life. If you spend time to be picky, you may become a 'mean' person. If you spend time to learn, you may gain wisdom. If you spend time with your family, you may foster a warm and loving relationship with your loved ones.

Friday, March 25, 2016

Wkb

Waholanzi walivyonaswa wakisafirisha Tumbili 61, uwanja wa ndege KIA. VYOMBO vya ulinzi na usalama katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) vimefanikiwa kuwanasa wafanyabiashara wawili ndugu, raia wa Uholanzi wakiwa katika harakati ya kusafirisha wanyama Hai 61,aina ya Tumbili kuelekea nchini Armenia. Wanyama hao wakiwa kwenye makasha sita tofauti ya kuhifadhia wanyama walikuwa wasafirishwe kwa ndege maalumu ya mizigo yenye namba EW/364G iliyosajiliwa nchini Belarus kupitia kampuni ya Arusha Freight Limited ya jijini Arusha. Raia hao wa Uholanzi waliokamatwa juzi majira ya saa 1:30 jioni katika uwanja wa ndege wa KIA wametambulika majina yao kuwa ni Arten Vardanian (52) aliyekuwa na hati ya kusafiria yenye namba NWF8CKJR8 na Edward Vardanian (46) aliyekuwa na hati ya kusafiria namba NY969P96.

Wkb

Zaidi ya watu 150 wajitokeza kuhakiki silaha zao. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna wa Polisi Diwani Athumani amesema hadi kufikia sasa zaidi ya watu 150 wamejitokeza kuhakiki wa silaha zao, katika hatua ya kutii agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. “Baada ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kufanya uhakiki wa silaha zake hivi karibuni, watu zaidi ya 150 wakiwemo viongozi mbalimbali waliopo Serikalini, Viongozi wastaafu, Mabalozi wa nchi mbalimbali, wafanyabiashara na wabunge wamejitokeza kuhakiki silaha zao, na wengine wameonesha nia ya kufanya hivyo, hata hivyo tusingependa kutaja majina yao kwa sababu za kiusalama” amesema Kamishna wa Polisi Athumani

Wednesday, March 23, 2016

Wkb

Mshukiwa aliyekuwa akisakwa sana kuhusiana na mashambulio ya Brussels amekamatwa na maafisa wa usalama, vyombo vya habari Ubelgiji vimeripoti. Baadhi ya vyombo vya habari limetaja jina lake kuwa Najim Laachraoui. Wadadisi wanasema Laachraoui anaaminika kuwa mtaalamu wa kuunda mabomu. Alionekana kwenye picha ya kamera za usalama uwanja wa ndege akiwa pamoja na washukiwa wawili ambao inadaiwa walijilipua wakati uwanja wa ndege wa Zaventem. Alikuwa tayari anatafutwa na polisi kuhusiana na mashambulio ya Paris mwaka jana. Ripoti za kukamatwa kwake bado hazijathibitishwa na maafisa wa usalama. Taarifa za awali zilikuwa zimewatambua washukiwa walioonekana naye kwenye uwanja wa ndege kuwa ndugu wawili, Brahim na Khalid El Bakraoui. Watu 34 walifariki na zaidi ya 250 kujeruhiwa kwenye mashambulio mawili yaliyotokea katika uwanja huo wa ndege wa Zaventem na kituo cha treni cha Maelbeek. Kundi linalojiita Islamic State limedai kutekeleza mashambulio hayo. Bendera zinapepea nusu mlingoti nchini Ubelgiji. Taifa hilo limetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa.

Tuesday, March 22, 2016

Wkb

#KutokaMagazetini - MWANDISHI ALIYETOWEKA, APATIKANA. Siku tatu baada ya mwandishi wa Mwananchi na DW, Salma Said kutoweka, jana alipatikana baada ya kukutwa katika Hospitali ya Regency ya jijini hapa na kupelekwa kituo kikuu cha polisi kuhojiwa. Habari zilizopatikana jana jioni na kuthibitishwa na mumewe, Ali Salim Khamis na Kamanda wa Kanda Maalumu ya Polisi, Simon Siro zilisema Salma alisajiliwa jana mchana katika hospitali hiyo. Ali aliyekuwa katika Kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam, alisema kwa ufupi kuwa amepata taarifa hizo na kufika Dar es Salaam kuzifuatilia. Kamanda Siro alisema ni kweli Salma amepatikana na ametumwa mkuu wa upelelezi wa kanda hiyo kumfuata hospitali ampeleke kituoni kwa mahojiano. Mpaka tunakwenda mitamboni Salma alikuwa anahojiwa. Awali, wadau wa habari waliungana na Kampuni ya Mwananchi Communications Limited (MCL), kueleza hofu yao kutokana na kutoweka kwa mwandishi wa habari, Salma Said na kuvitaka vyombo vya dola kulitafutia ufumbuzi wa haraka suala hilo. Mkurugenzi Mtendaji wa MCL, inayochapisha magazeti ya Mwananchi, The Citizen na MwanaSpoti, Francis Nanai alisema wanaendelea kufuatilia kwa makini suala hilo. “Taarifa za kutoweka kwa Salma zilitufikia Ijumaa mchana Machi 18, 2016 kupitia kwa mume wake, mpaka sasa hakuna taarifa yoyote inayoonyesha ni nani au chombo gani kinamshikilia au kumhifadhi, hali hii inatutia wasiwasi mkubwa kama kampuni na wadau wa habari nchini,” alisema Nanai. Wakati huo huo, Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni katika tamko lake ililolitoa jana ilieleza kuwa kutekwa kwa mwanahabari huyo kumezua maswali mengi kwa wananchi, familia yake, wadau na wanahabari wa ndani ya nchi na wale wa jumuia za kimataifa. “Kutekwa kwa Salma kunatokana na kazi yake ya uanahabari, ndiyo maana ushahidi wa awali uliopatikana kwa njia ya ujumbe wa sauti ukiwa na sauti inayoaminika kuwa ni yake, ulieleza wazi kutekwa kwake kunatokana na yeye kuripoti dosari zinazoendelea katika uchaguzi wa marudio Zanzibar,” alisema Joseph Mbilinyi, Waziri Kivuli wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo wa Kambi ya Upinzani. #Mwananchi