Sunday, July 23, 2017

Tetesi za soka

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 23.07.2017
Barcelona wapo tayari kutoa pauni milioni 80 kumtaka Philippe Coutinho, 25, kutoka Liverpool. (Sunday Mirror)

Mshambuliaji wa Barcelona, Lionel Messi, 30, ameiambia klabu yake kumsajili mshambuliaji wa Juventus Paulo Dybala, 23. (Don Balon)

Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema Coutinho “ametulia” Liverpool baada ya klabu hiyo kuzungumza naye kufuatia hatua ya Barcelona kumtaka. (ESPN FC)

Liverpool hatimaye wamefikia makubaliano na RB Leipzig ya pauni milioni 75 ili kumsajili Naby Keita. (Winner Sports)

Meneja wa Arsenal amekanusha taarifa kuwa Alexis Sanchez, 28, anakaribia kuhamia Paris Saint-Germain kwa pauni milioni 70. (Standard)

Alexis Sanchez anataka mshahara wa pauni 500,000 kwa wiki kutoka Paris Saint-Germain, huku akikaribia kuhamia Paris. (The Mirror)

Liverpool na Arsenal wameonesha dalili za kutaka kumsajili mshambuliaji wa Real Madrid Lucas Vasquez. (Diario Madridista)

Chelsea wanapanga kuzungumza na Arsenal kuhusiana na Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Sky Sports)

Chelsea wanamfuatilia winga wa Montreal Impact Ballou Jean-Yves Talba, baada ya Didier Drogba kuwaambia kuhusu mchezaji huyo. (Sun)

Manchester United wana uhakika wa kumsajili kiungo wa Chelsea Nemanja Matic, 28, baada ya kumkosa Eric Dier, 23, wa Tottenham. (Guardian)

Mipango ya Manchester United kutaka kumsajili kiungo wa PSG, Marco Verratti, 24, kwa pauni milioni 60 imesitishwa kwa muda baada ya PSG kusema inamtaka Anthony Martial, 21. (Sunday Mirror)

Jose Mourinho amesema “ana uhakika” David de Gea atabakia Manchester United msimu huu, baada ya Real Madrid kushindwa kutumia nafasi ya kumsajili kipa huyo. (Sky Transfer Centre)

Manchester United sasa wamemgeukia kiungo wa Bayern Munich, Arturo Vidal, wakati wakitafuta kiungo mpya. (Daily Star)

Beki wa Manchester United Matteo Darmian, 27, amesema haendi popote licha ya taarifa kumhusisha na kurejea Italy. (Press Association)

Real Madrid wametengeneza orodha ya washambuliaji inayowataka, ikiwa watamkosa Kylian Mbappe. Miongoni mwao ni Marcus Rashford wa Manchester United, Pierre Emerick-Aubameyang wa Borussia Dortmund na Timo Werner wa RB Leipzig. (Diario Gol)

Real Madrid watamsajili mshambuliaji wa Ajax Kasper Dolberg pamoja na Domenico Berardi wa Sassuolo, iwapo watamkosa Kylian Mbappe. (Marca)

Real Madrid wamewaambia Monaco watawapa Karim Benzima kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Kylian Mbappe. (The Sun)

Chelsea wamemuulizia winga wa Inter Milan Antonio Candreva, ili kuogeza ushindani Stamford Bridge. (the Sun)

Kiungo wa Manchester City Kevin de Bruyne, 26, amesema ana matumaini klabu yake itanunua mabeki wengine kadhaa msimu huu. (Manchester Evening News)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na Jumapili njema.

No comments:

Post a Comment