Friday, July 14, 2017

Tetesi

TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 14.07.2017
Liverpool na Chelsea wanataka kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Pierre Emerick-Aubameyang, 28, ambaye thamani yake ni pauni milioni 65. (Sun)

Dortmund wamemuambia Aubameyang kuamua anataka kwenda wapi kabla klabu hiyo haijaingia kambini nchini Uswisi Julai 24. (Sun)

Kipa wa Manchester United David de Gea, 26, anataka kujiunga na Real Madrid msimu huu na amemuambia wakala wake Jorge Mendes kufanikisha uhamisho wake. (Don Balon)

Manchester City wapo tayari kutoa pauni milioni 50 kumsajili beki wa kushoto wa Monaco, Benjamin Mendy, 22. (Daily Mirror)

Chelsea watakamilisha usajili wa kiungo Tiemoue Bakayoko, 22, kutoka Monaco kwa pauni milioni 39.7 katika saa 24 zijazo, ingawa mchezaji huyo atakosa mechi kadhaa za mwanzo kutokana na kuwa majeruhi. (Daily Express)

RB Lepzig wamekataa dau la pauni milioni 57 kutoka Liverpool la kumtaka kiungo Naby Keita, 22. (Bild)

Kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, atakataa kwenda Leicester kwa sababu anataka kujiunga na Everton. (Leicester Mercury)

West Ham wanakaribia kukamilisha usajili wa mkopo wa kipa wa Manchester City Joe Hart, 30. (Independent)

Newcastle watapewa nafasi ya kumsajili kipa wa West Ham Darren Randolp, ikiwa Joe Hart atakwenda West Ham. (Newcastle Chronicle)

Barcelona wameacha kumfuatilia beki wa Arsenal Hector Bellerin, 22, baada ya klabu hiyo ya Uhispania kufikia makubaliano ya kumsajili Nelson Semedo, 23 kutoka Benfica. (London Evening Standard)

Roma wametoa dau la pauni milioni 29 kumtaka Riyad Mahrez, 26, lakini Leicester wanataka pauni milioni 50. (London Evening Standard)

Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anataka uhamisho wa Kyle Walker, 27, kwenda Man City uharakishwe ili wapate fedha za kusajili wachezaji wengine. (Daily Mail)

Tottenham wanatarajia kuziba pengo la Kyle Walker kwa kumsajili beki wa Porto Rocardo Pereira, 23, kwa pauni milioni 22. (Times)

Tottenham wanakaribia kukamilisha usajili wa beki Juan Foyth, 19, kutoka Estudiantes, ambaye atakuwa usajili wa kwanza wa Spurs msimu huu. (ESPN)

Tianjin Quanjian wamempa mkataba wa pauni milioni 26 kwa mwaka, mshambuliaji wa Real Madrid Alvaro Morata, 24. (Onda Cero)

Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Ijumaa Kareem.

No comments:

Post a Comment