Friday, March 25, 2016

Wkb

Zaidi ya watu 150 wajitokeza kuhakiki silaha zao. Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Kamishna wa Polisi Diwani Athumani amesema hadi kufikia sasa zaidi ya watu 150 wamejitokeza kuhakiki wa silaha zao, katika hatua ya kutii agizo la Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda. “Baada ya Mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli kufanya uhakiki wa silaha zake hivi karibuni, watu zaidi ya 150 wakiwemo viongozi mbalimbali waliopo Serikalini, Viongozi wastaafu, Mabalozi wa nchi mbalimbali, wafanyabiashara na wabunge wamejitokeza kuhakiki silaha zao, na wengine wameonesha nia ya kufanya hivyo, hata hivyo tusingependa kutaja majina yao kwa sababu za kiusalama” amesema Kamishna wa Polisi Athumani

No comments:

Post a Comment